Friday, August 15, 2014

KATIBU MKUU WIZARA YA NISHATI NA MADINI ELIAKIM MASWI AFUNGUA SEMINA KWA MAKAMISHNA WASAIDIZI WA MADINI INAYOENDESHWA NA TANSORT BAGAMOYO

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi amefungua mafunzo yaliyoshirikisha Makamishna Wasaidizi wa Madini wa Kanda, Afisa Madini  Wakazi na  Wataalamu  kutoka Wizara ya Nishati na Madini mjini Bagamoyo
Picha Na. 1
Mkurugenzi wa Kitengo cha  Uchambuzi na Uthamini wa Madini ya Almasi na Vito, (TANSORT) kilichopo chini ya Wizara  ya Nishati na Madini   Archard Kalugendo  akiwasilisha mada kwenye semina  iliyoshirikisha Makamishna Wasaidizi wa Madini wa Kanda,  Afisa Madini Wakazi na  Wataalamu wa Wizara ya Nishati na Madini inayoendelea Bagamoyo  yenye lengo la  kujadili utendaji na  uboreshaji wa  shughuli za uthaminishaji wa madini ya almasi na vito nchini.
Picha Na 2
Kaimu Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Mashariki  (kushoto) Elias Kayandabila akifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zinawasilishwa.
Picha Na 3  
Mtaalamu kutoka Kitengo cha TANSORT Teddy  Goliama  akisisitiza jambo wakati wa semina hiyo
Picha Na 8
Kamishna wa Madini, Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi  Paul Masanja akizungumza kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa Nishati na Madini Eliakim Maswi ali aweze kufungua semina hiyo
Picha Na 9
Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi akifungua semina hiyo
Picha Na. 6
Baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakifuatilia  kwa makini mada zilizokuwa zinawasilishwa katika semina hiyo
Picha Na. 7
Mkurugenzi wa Kitengo cha TANSORT, Archard Kalugendo  (wa kwanza kushoto) Afisa Rasilimaliwatu Lameck Kabeho (katikati) na Kamishna Msaidizi wa Madini- Sehemu ya Uongezaji Thamani Mwacha Mtoro wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zinawasilishwa na mtoa mada (hayupo pichani)
Picha Na. 10
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi ( wa nne kutoka kushoto waliokaa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa semina hiyo
Picha Na 4
Mtaalamu kutoka Kitengo cha TANSORT Teddy  Goliama  akisisitiza jambo wakati wa semina hiyo
Picha Na 5
Mtaalamu kutoka  TANSORT Edwin Rweyemamu akichangia  hoja  katika moja ya mada zilizowasilishwa katika semina hiyo

No comments: