Friday, August 29, 2014

RAIS KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA MBANDE-KONGWA 16.5KM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi, Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakwanza kushoto akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi pamoja na Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai wakifurahia mara baada ya Rais kuweka jiwe la Msingi Ujenzi wa Barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km .
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma pamoja na kikundi cha ngoma za asili cha Kibaigwa kabla ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuhutubia mamia ya Wakazi wa Kibaigwa.
Sehemu ya barabara Mbande-Kongwa 16.5Km ambayo ujenzi wake umewekwa jiwe la Msingi.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kulia akizungumza na Mbunge wa Kibakwe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa George Simbachawene huku Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai akishuhudia kushoto.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katikati akizungumza na Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya(kulia) kabla ya uzinduzi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya uzinduzi na ufunguzi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.
Viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zake wakimsubiri Rais Dkt. Jakaya Kikwete kuzindua rasmi mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km. Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi

No comments: