Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Kyando Mchechu akizungumza
katika hafla hiyo mchana huu.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Kyando Mchechu akizungumza
katika hafla hiyo mchana huu.
Baadhi
ya watendaji wa NHC wakifuatilia jambo kwenye hafla hiyo, Kushoto ni Susan
Omari, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa NHC, Muungano
Saguya, Meneja Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa NHC, Mkurugenzi wa
Uendelezaji Biashara wa NHC, David Shambwe, Meneja Mauzo wa NHC, Tuntufye
Mwambusi na Meneja Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu, Bulla Boma.Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Kyando Mchechu akitiliana saini hati ya makubaliano na Afisa Mtendaji Mkuu wa Uchumi, Dk. Jonathan Ciano.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Kyando Mchechu wakibadilishana hati ya makubaliano na Afisa Mtendaji Mkuu wa
Uchumi, Dk. Jonathan Ciano.
**********************************************************
SHIRIKA
la Nyumba la Taifa (NHC) na Uchumi Supermarkets Tanzania Limited (USL), leo
mchana wametiliana saini makubaliano yatakaziwezesha pande hizo mbili
kushirikiana kibiashara ambapo USL itapewa kipaumbele kwenye kupanga katika
miradi ya ujenzi ya majengo ya Shirika la Nyumba la Taifa popote nchini.
Akizungumza
wakati wa hafla ya utiaji saini hati ya makubaliano kati ya Shirika la Nyumba
la Taifa (NHC) na Uchumi Supermarkets Tanzania Limited (USL), Mkurugenzi Mkuu
wa Shirika la Nyumba alisema makubaliano hayo yataziwezesha pande hizo mbili kufaidika
na makubaliano hayo.
“Tunachkishuhudia
hapa Serena leo ni makubaliano kati ya pande mbili hizi yatakayowezesha kukuza
biashara nchini na hivyo kuwafanya Watanzania wengi zaidi kuimarika kiuchumi
kwani NHC itafungua fursa kwa uchumi na Uchumi pia watafungua fursa kwa NHC.
Miaka ya nyuma kidogo nilipokwenda Kenya nilivutiwa na namna ambavyo Uchumi
wanakuza uchumi wa Kenya kwa kununua bidhaa za wakulima wa Kenya, natarajia
kile kilichofanyika kule kitafanyika hapa Tanzania pia, kwani ukuaji wa biashara
na pesa hauna mipaka,”alisema.
Alisema
kwa Uchumi imeweza kutumia fursa hiyo itakayoiwezesha kupata kipaumbele kwenye
miradi ya majengo ya biashara popote pale Tanzania na akatoa wito kwa taasisi,
mashirika na vyombo vingine kutumia fursa hiyo ili uchumi wan chi uweze kukua.
Naye
Mtendaji Mkuu wa Uchumi, Dk. Jonathan Ciano alisema kuwa Kampuni yake
imefurahishwa kuingia katika makubaliano hayo ambayo yataiwesha sasa kupata
maeneo bora ya kufanyia biashara kwani wameweza kuingia makubaliano na
mwendelezaji nambari moja wa miliki ambaye ataweza kuwapa maeneo mazuri kwajili
ya uwekezaji kibiashara.
Alisema
watayaenzi makubaliano hayo na hivyo kumudu
kukuza uchumi wa Watanzania kwa kuweza kununua bidhaa zao na kuziuza
kwenye Supermarkets zao.
Hafla
hiyo ilihudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwamo watendaji wa Mamlaka ya ukuzani
mitaji na masoko nchini na wadau wengine mbalimbali.
No comments:
Post a Comment