Tuesday, August 26, 2014

RAIS KIKWETE ATUNUKU KAMISHENI TMA MONDULI

D92A6383
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mkuu wa majeshi wa kwanza Mzalendo Jenerali Mirisho Sarakikya muda mfupi baada ya kuwasili katika chuo cha jeshi Monduli tayari kwa kutunuku kamisheni kwa maofisa 179 wapya wa jeshi waliohitimu vyema mafunzo yao mwishoni mwa wiki.
D92A6430
Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama Jenerali Davis Mwamunyange kushoto na Mkuu wa Chuo cha Jeshi (TMA) Monduli Brigedia Jenerali Paul Peter Massao(kulia) wakimsindikiza Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho kwenda uwanja wa Paredi ambapo alitunuku kamisheni kwa maofisa wapya wa jeshi katika sherehe zilizofanyika katika chuo cha jeshi(TMA) mkoani Arusha.
D92A6441
Mkuu wa Chuo Cha Jeshi Monduli TMA Brigedia Jenerali Paul Peter Massao akimsindikiza Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuingia katika viwanja vya Paredi chuoni hapo akiwa katika gari maalumu ambapo alitunuku kamisheni kwa maofisa wapya wa Jeshi.
D92A6497
Mkuu wa Chuo Cha Jeshi Monduli TMA Brigedia Jenerali Paul Peter Massao akimsindikiza Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuingia katika viwanja vya Paredi chuoni hapo akiwa katika gari maalumu ambapo alitunuku kamisheni kwa maofisa wapya wa Jeshi.
D92A6512
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea salamu ya heshima mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Paredi kutunuku kamisheni katika chuo cha jeshi Monduli mkoani Arusha Jumamosi.
D92A6553
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua vikosi hkwenye  uwanja wa Paredi la kutunuku kamisheni katika chuo cha jeshi Monduli mkoani Arusha Jumamosi.
D92A6628
Maofisa Wapya wa jeshi wakipita mbele ya mgeni Rasmi Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na kutoa heshima wakati wa gwaride maalumu la Kamisheni lilofanyika katika chuo cha TMA Monduli.
D92A6697
Kikosi cha Bendera kikipita  mbele ya Amiri jeshi mkuu Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  wakati wa gwaride maalumu la Kamisheni lilofanyika katika chuo cha TMA Monduli.
D92A6761
Maofisa Wapya wa jeshi wakipita mbele ya mgeni Rasmi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete nakutoa heshima wakati wa gwaride maalumu la Kamisheni lilofanyika katika chuo cha TMA Monduli.

No comments: