Friday, August 29, 2014

SKYLIGHT BAND WAZIDI KULITIKISA JIJI LA DAR NA VIUNGA VYAKE KWA BURUDANI KALI

Diva wa Skylight Band Mary Lucos akiimba kwa uzuri kabisa Ndani ya kiota cha burudani Thai Village. Bendi yako machachari na inayopendwa zaidi ndani ya Jiji la Dar es salaam na viunga vyake vyote Skylight Band inakukaribisha wewe mdau,mpenzi na shabiki wa kweli Leo hii kuanzia mida ya Tatu kamili ndani ya ukumbi wa Thai Village Masaki,ambapo burudani ya nguvu itaporomoshwa na wanamuziki mahiri wa bendi hiyo kama Aneth Kushaba, Mary Lucos, Digna Mbepera, Sam Machozi, Donode, Joniko Flower na Sony Masamba. Njoo upate muziki mzuriiiii na ladha zote za kiafrika na ulaya pamoja na suprizeee kibaooooo.
Digna Mbepera akiimba na kucheza kwa umahiri kabisa ili kuwapa burudani wapenzi na mashabiki wake.
Anaitwa Aneth Kushaba a.k.a AK47 au Le Meneja Her Self akiimba kwa mikogooo safi ndani ya Thai Village ili kuwapa burudani ya nguvu mashabiki wake.
Le Meneja Her Self akiimba kwa hisia kaliiiiii kabisaaaaa.
Aneth Kushaba(katikati)akiongoza madiva wenzake wa Skylight Band Digna Mbepera(kulia) na Mary Lucos(kushoto) kushambulia jukwaaa sawa sawa na kwa vocal kali.
Hashimu Donode A.K.A Dogo Dogo akilishambulia jukwaaa kwa nguvu ili kuwapa burudsni mashabiki wake.
Bana ba Kongo Joniko Flower(kushoto) na Sony Masamba(kulia) wakiimba kwa uzuriiiii kabisa zile ladha za kilingala na bolingo na kutoa burudani kaliiii kwa mashabiki wa Skylight Band
Hapo sasaaaa Bana ba Kongooo wakianza kuyarudi mauno taratibuuuuuuu
Joniko Flower(kushoto)akiongoza Majembe ya Skylight Band Sony Masamba(katikati) na Sam Mapenzi(kulia)kucheza masebene yaliyokuwa yakiporomoshwa ndani ya Thai Village

No comments: