Saturday, August 02, 2014

CCM YASTUKIA USANII WA UKAWA

     Chama Cha Mapinduzi kimewastukia Ukawa na kusema wanachofanya
ni Usanii usiokuwa na tija mbele ya mambo ya msingi kwa Taifa la Tanzania,
akizungumza na mwaandishi wa habari hizi Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM
Nape Nnauye alisema hoja zote zinazotolewa na UKAWA zina majibu kwenye Sheria na
Kanuni zinazoendesha Bunge la Katiba ,CCM pia imewashukia  UKAWA kwa kuwatukana na kuwadhalilisha
viongozi wa dini ambao wamekuwa wakisisitiza UKAWA kurudi Bungeni.
     CCM yawaomba wabunge wa bunge la Katiba wanaotaka Katiba
mpya waendelee na bunge  litakapoitishwa
tarehe 5/8/2014.
Kwa taarifa za ndani ya kikao hicho ,kikao kimeisha kwa
kukubalina kutokubaliana ,pande mbili hizi zimekutana zaidi ya mara nne pamoja
na kikao cha leo kilichoanza tangia asubuhi saa nne mpaka jioni lakini hakuna
hata pande mmoja uliokubalina na mwenzake.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani Msajili wa vyama vya
Siasa  nchini anatarajiwa kuzungumza na
waandishi wa habari kesho jijini Dar es Salaam.

No comments: