Thursday, September 04, 2014

YOUNG AFRICANS NA BENKI YA CRDB WAINGIA MAKUBALIANO YA UTENGENEZAJI WA KADI ZA KISASA ZA UANACHAMA


 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei (kulia) akisaini mkataba na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Klabu ya Yanga, Fatma Karume kwa ajili ya kutengeneza kadi za kisasa za uanachama wa klabu hiyo za mfumo wa kieletroniki 'Gold Premium Card'. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa klabu ya Yanga, Mama Fatma Karume akipitia mkataba walioingia na Benki ya CRDB. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akionyesha kadi ya kisasa ya uanachama wa Yanga ikiwa katika mfumo wa kieletroniki kabla ya kumkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa klabu hiyo, mama Fatma Karume.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei (kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Yanga,  Fatma Karume kadi namba moja ya mfumo wa kieletroniki 'Gold Premium Card' mara baada ya benki hiyo kuingia mkataba wa kutengeneza kadi hizo. Hafla hiyo ilifanyika Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Dar es Salaam. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Yanga,  Fatma Karume akizungumza katika hafla hiyo. 
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay. (katikati)
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei  akizungumza wakati wa hafla hiyo.

No comments:

RAIS DKT. MWINYI: MUUNGANO UENDELEE KUWA CHACHU YA UKUAJI WA UCHUMI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa ushirikiano uliopo kati ya Serikali ya Map...