Monday, September 22, 2014

GREEN WASTE PRO LTD WAKAMILISHA KAMPENI YA USAFI KWA UFANISI, TICTS NAO WASHIRIKI‏

DSC_0005
Baadhi ya wafanyakazi Kampuni ya Kupakua na Kupakia Kontena Bandarini (TICTS) wakiwasili kwenye ufukwe wa bahari ya hindi maeneo Kata ya Kivukoni kwa ajili ya kushiriki zoezi la kusafisha fukwe hizo katika kuhitimisha kampeni usafi iliyokuwa ikiendeshwa na Kampuni ya Green Waste Pro Ltd mwishoni mwa juma.
DSC_0028
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya TICTS, kampuni ya usafi ya Green Waste Pro Ltd na watendaji wa halmashauri pamoja na viongozi wa kata ya Kivukoni wakichukua vitendea kazi tayari kuanza kusafisha fukwe za bahari ya hindi.
DSC_0034
Meneja Kitengo cha Makontena TICTS, Bw. Donald Talawa (kulia), akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ushiriki wao kwenye zoezi la kusafisha mazingira yanayozunguka fukwe za bahari ya hindi kata ya Kivukoni lililokuwa likiendeshwa na kampuni iliyopewa zabuni ya kusafisha manispaa ya Ilala Green Waste Pro Ltd. Katikati ni Meneja wa mwendeshaji wa kampuni ya Green Waste Pro Ltd, Abdallah Mbena na Kushoto ni Afisa Mtendaji wa Kata ya Kivukoni Bw. Renatus Ruhungu.
DSC_0041
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya TICTS wakimsikiliza Meneja Kitengo cha Makontena TICTS, Bw. Donald Talawa (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye maeneo ya fukwe za bahari ya hindi zilizopo katika Kata ya Kivukoni.
DSC_0045
Afisa Mtendaji wa Kata ya Kivukoni Bw. Renatus Ruhungu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) ambapo alitoa pongezi kwa kampuni ya Green Waste Pro Ltd kwa kuifanya manispaa ya Ilala kuwa safi na kutaka kampuni zingine za usafi kuiga mfano wa kampuni hiyo na kuwaasa wananchi kutoa ushirikiano wa masuala ya usafi wa mazingira kwa sababu ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha mazingira yetu yanayotuzunguka yanakuwa safi wakati wote.
DSC_0070
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya TICTS na Green Waste Pro Ltd wakishirikiana kusafisha fukwe za bahari ya hindi wakati wa kuhitimisha kampeni ya usafi iliyokuwa ikiendeshwa na Green Waste Pro Ltd.
DSC_0078
Kulia ni Meneja uhusiano wa TICTS, Jema Kachota na mfanyakazi mwenzake wakielekea kushiriki zoezi la kusafisha fukwe hizo lililokuwa likiendeshwa na kampuni ya Green Waste Pro Ltd ambapo TICTS nao waliunga mkono kampeni hiyo iliyofikia tamati mwishoni mwa juma.
DSC_0096
Meneja Kitengo cha Makontena TICTS, Bw. Donald Talawa (kulia) akivaa glovu tayari kushiriki zoezi la kusafisha mazingira yanayoizunguka bahari ya hindi katika Kata ya Kivukoni mwishoni mwa juma. wengine ni baadhi ya wafanyakazi wa TICTS.
DSC_0109
Meneja Kitengo cha Makontena TICTS, Bw. Donald Talawa akishiriki kuzoa uchafu uliotapakaa kwenye fukwe hizo akishirikiana na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Green Waste Pro Ltd pamoja na wafanyakazi wenzake.

No comments: