Tuesday, September 30, 2014

BALOZI WA JAPAN ZIARANI WILAYANI MONDULI

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa
akimkaribisha wilayani Monduli Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh.  Masaki Okada wakati alipowasili wilayani humo juzi Jumapili Septemba  28,2014 kwa ajili ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na nchi hiyo.Balozi huyo aliahidi kusaidia vifaa vya  kisasa katika hospitali mpya ya kisasa inayojengwa wilayani humo.
Meneja wa Hoteli ya Emanyata mjini Monduli,Bi. Neema (kushoto) akimkaribisha  Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaki Okada hotelini hapo.Pembeni  kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Monduli,Bw. Twalib  Mbasha.
Balozi wa Japan nchini,Mh. Masaki Okada (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Monduli,Twalib Mbasha (kulia) na Meneja wa  Hoteli ya Emanyata mjini Monduli,Bi. Neema alikofikia balozi huyo na 
ujumbe wake katika ziara yake ya siku mbili wilayani humo

No comments:

WAZIRI NA NAIBU WAZIRI WA ARDHI WASHIRIKI KIKAO CHA KWANZA CHA MKUTANO WA 19 WA BUNGE LA 12 KWA AJILI YA KUJADILI BAJETI YA SERIKALI 2025/2026

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi (MB), leo tarehe 8 Aprili 2025, ameshiriki kikao cha kwanza cha Mku...