Tuesday, September 30, 2014

ABDULRAHMAN KINANA NA WANA BUMBULI WATETA, DIWANI AFUKUZWA MKUTANONI NA WANANCHI

1Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Mbunge wa jimbo la Bumbuli na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Mh. Januari Makamba wakati alipowasili  katika kata ya Mbuzii ambapo ameshiriki katika ujenzi wa ofisi ya tawi la CCM katika kata hiyo na kuzungumza na wananchi waliojitokeza kumpokea, Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana yuko katika ziara ya kikazi mkoa wa Tanga akihimiza na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 na kukiiarisha chama akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi Chama cha Mapinduzi CCM, Kero kubwa katika mkutano huo ilikuwa ni kufungwa kwa kiwanda cha Chai cha Mponde ambacho wananchi wanataka warudishiwe ili wakiendeshe wenyewe ,Baada ya mwekezaji Yusuf Mulla kukiuka makubaliano ya kisheria jambo lililopelekea mmoja wa viongozi katika kata hiyo ambaye ni diwani Diwani wa Kata ya Guga Bw. Richard Mbunguni kufukuzwa mkutanoni na wananchi mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwa madai ya kuwasaliti katika sakata hilo, Akizungumza na wananchi katika kutano huo  Kinana ameahidi kulifuatilia suala hilo kwa ukaribu akisema “Katika hili kila mtu aliyehusika abebe mzigo wake kwa kuwajibika” , ameahidi kurudi Mponde baada ya mwezi mmoja ili kuwapatia majibu sahihi wananchi yatakayomaliza kabisa mgogoro huo.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-BUMBULI -LUSHOTO)2Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza  Mbunge wa jimbo la Bumbuli na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Mh. Januari Makamba alipokuwa akizungumza na jambo wakati alipowasili  katika kata ya Mbuzii.3Mbunge wa jimbo la Bumbuli na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Mh. Januari Makamba  akizungumza na wanapiga kura wake wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanaalipowasili  katika kata ya Mbuzii.4Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akishiriki ujenzi wa ofisi ya CCM tawi la Mbuzii wakati  akiwa katika ziara ya kikazi katikajimbo la Bumbuli, Kulia anayeangalia ni Mbunge wa jimbo la Bumbuli na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Mh. Januari Makamba.5Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akizungumza na vijana wa kikundi cha Bodaboda cha Dule B wakati alipozindua tawi lao na kukabidhi pikipiki iliyotolewa kwa kikundi hicho na mbunge wa jimbo hilo Mh. Januari Makamba katikaki pichani na kushoto ni  Mkuu wa wilaya ya Lushoto Mhe. Majid Hemed Mwanga.6Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akikabidhi fungua za pikipiki kwa kiongozi wa kikundi cha Dule B Bw.Nuru ambayo imetolewa na Mbunge wa jimbo la Bumbuli Mh. Januari Makamba.7Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akizungumza na wanakikundi cha Maisha Plus wakati alipotembelea kikundi hicho.8Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akishiriki kazi ya kuponda kokoto wakati alipotembelea kikundi cha Maisha Plus ambacho hii ni moja ya kazi zinazofanywa na kikundi hicho.9Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa. Itikadi na Uenezi Chama cha Mapinduzi akishiriki kazi ya kufyatua matofari huku mbunge wa jimbo hilo Mh. Januari Makamba akishuhudia wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipokitembelea kikundi cha wajasiriamali cha Maisha Plus.10Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa. Itikadi na Uenezi Chama cha Mapinduzi akiendelea na kazi ya kufyatua matofali11Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akila muwa na Mwandishi wa habari wa kituo cha Televisheni cha ITV Ufoo Sari wakati alipotembelea kikundi cha wajasiriamali cha Maisha Plus jimboni Bumbuli leo miwa hiyo inazalishwa na kikundi hicho.12Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akiranda mbao huku Mbunge wa jimbo la Bumbuli Mh. Januari Makamba akishuhudia13Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  ameshiriki pia kuchoma tanuri la matofari kwa kuwasha moto katika moja ya matundu ya tanuri hilo anayeangalia ni Mbunge wa jimbo la Bumbuli Mh. Januari Makamba .14Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati akizungumza jambo na mbunge wa jimbo la Bumbuli Mh. Januari Makamba15Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa. Itikadi na Uenezi Chama cha Mapinduzi CCM akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kata ya Mponde.16Mbunge wa jimbo la Korogwe Vijijini na Mchumi wa mkoa wa Tanga CCM akiwasalimia wananchi kwenye mkutatano wa hadhara uliofanyika kata ya Mponde jimbo la Bumbuli.17Baadhi ya wananchi wakiwa wamefurika kwa wingi katika mkutano huo.18Baadhi ya wananchi wakiwa wamefurika kwa wingi katika mkutano huo.19Baadhi ya wananchi wakiwa wamefurika kwa wingi katika mkutano huo.20Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa. Itikadi na Uenezi Chama cha Mapinduzi CCM akisisitiza jambo wakati akiwahutubia wananchi.21Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kata ya Mponde.23Mbunge wa jimbo la Bumbuli Mh. Januari Makamba akizungumza na wapiga kura wake katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Mponde jimboni Bumbuli.24Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa. Itikadi na Uenezi Chama cha Mapinduzi CCM akimtoa katika eneo la mkutano huku akiwa amemshika mkono diwani wa Kata ya Guga Bumbuli  Bw. Richard Mbuguni kulia aliyefukuzwa na wananchi katika mkutano huo wa hadhara  kwa madai ya kuwasaliti na kushirikiana na mwekezaji .

No comments: