Monday, September 29, 2014

KINANA AIBOMOA CHADEMA LUSHOTO, KAGONJI NA WAFUASI WAKE WAREJEA CCM

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto) akimkabidhi kadi ya CCM aliyekuwa mgombea ubunge Jimbo la Mlalo kupitia Chadema, Charles Kagonji aliyetangaza kukihama chama hicho na kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Sunga, Jimbo la Mlalo, Lushoto, Mkoa wa Pwani jana. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Lushoto, Balozi Abdi Mshangama

Kagonji ni mwanasiasa mkongwe ambaye kabla ya kuhamia Chadema aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Mlalo. Pia baadhi ya viongozi wa Chadema akiwemo Katibu wa Jimbo la Lushoto, Ismail Semkunde wamejiunga na CCM. PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG


 Kinana akikumbatiana kwa furaha na Kagonji. Kinana akiwa Mbunge wa Jimbo la Arusha, Kagonji naye alikuwa Mbunge wa Jimbo la Mlalo.
 Kinana akizungumza jambo na Kagonji
 Kagonji akihutubia mkutano wa hadhara baada ya kutangaza uamuzi wake wa kurejea CCM
Aliyekuwa Katibu wa Chadema Jimbo la Lushoto, Ismail Semkunde (kulia) akipongezwa na Kinana baada ya kujiunga na CCM.

No comments: