Saturday, September 27, 2014

KAMATI ZAPENDEKEZA KUANZISHWA TUME YA WALIMU NA NYINGINE

CHAZBaadhi ya Kamati za Bunge Maalum la Katiba zimependekezwa kuwepo kwa Ibara mpya inayohusu kuanzishwa kwa Tume za Huduma  za Sekta, mbalimbali  ikiwemo  ya Afya, Elimu , Walimu  na nyinginezo ili kuweza kukabiliana  na matatizo yanayowakumba.
 Kamati hizo zimependekeza  suala hilo, katika sura ya 13 na 14  ya Rasimu ya Katiba inayopendekezwa.
Hayo yamebainika leo wakati wa uwasilishaji wa taarifa  za Kamati Namba Moja hadi Kamati Namba Kumi na Mbili za Bunge hilo kuhusu uhakiki wa Rasimu hiyo  uliofanyika  kwenye kikao cha arobaini na tatu kilichofanyika mjini Dodoma.
 Taarifa hizo,ambazo zimewasilishwa na baadhi ya wenyeviti wa Kamati hizo na baadhi ya wajumbe kutoka 201  waliopewa ridhaa  za kuwasilisha.
 Baadhi ya Kamati  za Bunge hilo,ambazo zimependekeza suala ni  Kamati  namba 5 na  6.
Akizungumzia kuhusu suala hilo, kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati  Namba Sita  ya Bunge hilo, mjumbe wa Bunge hilo, Charles Mwaijage  alisema Kamati  yake inapendekeza kuongeza Ibara mpya ya 208A mara baada ya Ibara ya 208 itakayosomeka kama ifuatavyo:
 “Kwa kuzingatia umuhimu wa sekta za huduma za jamii kwa wananchi, Bunge litatunga sheria ya kuanzisha Tume za Huduma za Sekta hizo, kwa ajili ya uendeshaji wa ufanisi zikiwemo za Elimu,Afya na nyingine kadri mahitaji yatakavyojitokeza ,” alisema Mwaijage.
 Kwa upande wa  Kamati Namba Tano ya Bunge Maalum la Katiba,mjumbe wa Bunge hilo, Paul Makonda akitoa taarifa hiyo kwa niaba ya Mwenyekiti alisema, Kamati hiyo inapendekeza katika sura ya 14 kuongezwa kwa kifungu kipya kitakachounda Tume ya Utumishi wa Walimu  na kusomeka :
 (1)Kutakuwa na Tume ya Utumishi wa Walimu itakayoshughulikia, mishahara, maslahi, ajira na masuala ya kinidhamu kwa walimu.
 (2)Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu muundo, majukumu  mambo mengine kuhusu utkelezaji wa Tume ya Utumishi wa Walimu.
 Akizungumzia kuhusu suala hilo, Ezekiah  Olouch, aliomba Kamati ya Uandishi ya Mhe.  Andrew Chenge  kuliangalia.  
 Alisema zawadi ambayo watamkumbuka na walimu, Mwenyekiti wa Bunge  hilo, Mhe. Samuel Sitta na Bunge hilo  kwa walimu  hao ni kuingizwa kwa tume hiyo ambayo itasaidia kutatua mattaizo ya walimu kwa asilimia 90.

No comments: