Tuesday, September 30, 2014

Shirika la Nyumba la Taifa lakabidhi mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana Kigoma

 Meneja wa Mkoa NHC, Nistas Mvungi akimkabidhi Mkuu wa Mkoa mashine 32 za kufyatulia matofali ya kufungamana.
  
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Ujiji akishukuru Shirika kwa kuwapatia vijana mashine ya hydraform.
  
Wafanyakazi wa NHC na kikundi cha Vijana Kwanza Group  na wageni waalikwa wakisubiria Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa Mhe Kanali Issa Machibya.
 Meneja wa Shirika la Nyumba Kigoma Ndg Nistas Mvungi akijadiliana na Mkuu wa Mkoa Mhe Issa Machibya jambo kuhusiana na Mashine ya matofali ya kufungamana kuhusu ufanisi wake na ajira kwa vijana.
 Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa Shirika Mkoa wa Kigoma na Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa Mhe Kanali Issa Machibya.
 Meneja wa Shirika la Nyumba Ndg. Nistas Mvungi akihutubia wananchi wa Kigoma kuhusu mradi wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana 32 zilizotolewa na Shirika kwa vikundi vya  vijana wa Mkoa wa Kigoma
 Mkuu wa Wilaya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Ramadhan Maneno akikabidhi mashine za kufungamana kwa Kikundi cha Vijana Kwanza Group. Mwenyekiti wa kikundi Ndg Daniel George  na Katibu wake wakipokea mashine.

  
Picha ya pamoja ya kikundi cha vijana kwanza group na mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa. 
Wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Ramadhani Maneno kwa makini kuhusiana na maelekezo yake kuhusu umuhimu wa kutumia matofali ya kufungamana na kuondokana na nyumba za matope.


No comments: