Thursday, April 10, 2014

Serikali yawataka waandishi wa habari kuzingatia weledi taaluma ya habari wanapotekeleza majukumu yao

 Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –Usajili wa Magazeti Bw. Raphael Hokororo (kulia) akisalimiana na Muhariri Mtendaji wa gazeti la The  Guardian Bw. Wallace Mauggo(kushoto) mara baada ya kuwasili kwenye chumba cha habari cha gazeti hilo leo jijini Dar es salaam. Katikati ni Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Assah Mwambene.
 Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Assah Mwambene (kulia) akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa magazeti ya The Guardian na Nipashe Bw. Kiondo Mshana (kushoto) alipomtembelea ofisini kwake eneo la Mwenge jijini Dar es salaam kwa lengo la kukuza ushirikiano na kujadili changamoto mbalimbali za tasnia ya habari hapa nchini.
 Mwandishi mwandamizi wa gazeti la Guardian Bw. Polycarp Machira (kushoto) na Naibu Muhariri wa gazeti hilo Bw. Wenceslaus Mushi wakifurahia jambo wakati wa mkutano kati ya watendaji wa magazeti ya Guardian na Nipashe na Idara ya Habari.
 Mpiga Picha Mkuu wa gazeti la Guardian Bw.Seleman Mpochi (kulia) na Muhariri mtendaji wa Gazeti la Nipashe Bi. Frola Wingia wakifuatilia mazungumzo ya Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Assah Mwambene alipozitembelea ofisi za magazeti hayo jijini Dar es salaam.

No comments: