Tuesday, April 08, 2014

Tanzania na Umoja wa Ulaya (EU) Ziliposaini Mkataba wa Kubadilishana Washitakiwa wa Uharamia

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe.  Bernard K. Membe (Mb) na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya wa Mambo ya Nje na Usalama, Bi. Catherine Ashton wakiweka saini  Mkataba wa Kubadilishana Maharamia wanaokamatwa Bahari Kuu. Mkataba huo ulisainiwa mjini Brussels, Ubelgiji hivi karibuni. Mhe. Membe alifwatana  na  ujumbe wa Rais kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Umoja wa Ulaya na Afrika unaofanyika mjini Brussels.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Benard K. Membe (Mb.) na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya wa Mambo ya Nje  na Usalama, Bi. Catherine Ashton wakipeana mkono mara baada ya kusaini mkataba huo.Picha Kutoka Wizara ya 
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

No comments: