Wednesday, April 30, 2014

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene amesema Jaji Joseph Warioba alitunukiwa tuzo ya muungano iliyotukuka kwa kuwa alistahili kupewa kama viongozi wengine na kuwa kitendo si kumkejeli kama baadhi ya vyombo vya habari vilivyoripoti hivi karibuni.

Mkurugenzi Idara ya Habari Assah Mwambene akitoa ufafanuzi mbele ya  Waandishi wa Habari (hawapo pichani) juu ya tuzo aliyopewa Jaji Joseph Sinde Warioba wakati wa Sherehe za Muungano, ufafanuzi huo umetolewa leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Idara ya Habari Assah Mwambene (kushoto) akijibu maswali mbalimbali wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) juu ya tuzo aliyopewa Jaji Joseph Sinde Warioba wakati wa Sherehe za Muungano. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Vicent Tiganya. Mkutano huo umefanyika leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam.
read more

No comments: