Thursday, April 10, 2014

Bunge la Katiba kuwaka moto upya wakati taarifa za Kamati zitakapoanza kuwasilishwa, huku mvutano mkubwa ukitarajiwa kuwa juu ya muundo wa Muungano.

Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samia Hassan Suluhu (kulia), akipokea ripoti ya Kamati Namba Tano ya Bunge hilo kutoka kwa Mwenyekiti wa kamati hiyo, Hamad Rashid Mohamed Mjini Dodoma jana. Picha na Salhim Shao  
---
Bunge la Katiba leo linatarajiwa kuwaka moto upya wakati taarifa za Kamati zitakapoanza kuwasilishwa, huku mvutano mkubwa ukitarajiwa kuwa juu ya muundo wa Muungano.
Katika taarifa hizo, wakati kundi la walio wengi hasa kutoka CCM wakionekana kupania kuifumua Rasimu ya Katiba na kuingiza maudhui ya Serikali mbili katika Sura ya Kwanza na ya Sita zinazohusu Muungano, walio wachache wanaitetea Rasimu na kuchambua kasoro lukuki za Muungano.
 
Habari kutoka katika kamati hizo, zinabainisha kundi la walio wachache limeandaa hoja nyingi kuliko za walio wengi kwa mfano, katika Kamati Namba Nne inayoongozwa na Christopher Ole Sendeka taarifa ya wengi ina kurasa 13 wakati taarifa za wachache iliyoandaliwa na Tundu Lissu ina kurasa 50.Kwa habari zaidi Bofya na Endelea.....

No comments: