Wednesday, April 16, 2014

MKE WA RAIS MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA RASMI UCHUNGUZI WA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI WILAYA YA BAHI - MKOANI DODOMA


 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akijumuika na wacheza ngoma na wananchi mbalimbali wa wilaya ya Bahi mara baada ya kuzindua rasmi upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi kwa akinamama.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokewa na Mkuu wa Wilaya ya Bahi Ndugu Betty Mkwasa mara baada ya kuwasili mjini Bahi kushiriki mkwenye sherehe ya uzinduzi wa uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi tarehe 14.4.2014
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, Mama Salma Kikwete akiwapungia wanafunzi na wananchi wa Bahi waliohudhuria sherehe ya uzinduzi wa saratani ya shingo ya kizazi mjini hapo tarehe 14.4.2014.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wananchi wa wilaya ya Bahi muda mfupi kabla ya kuzindua rasmi kampeni ya upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake katika wilaya ya Bahi mkoani Dodoma.
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kampeni ya kutokomeza saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake wa Wilaya ya Bahi.
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akionyesha vifaa mbalimbali vinavyotumika na madaktari wakati wa kuwapima wanawake ili kufahamu kama wana maambukizi ya saratani ya shingo ya kizazi wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo wilayani Bahi.
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Mganga wa Macho wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Frank Magupa, wakati alipotembelea maonesho ya kitabibu yaliyofanyika sambamba na upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake wa wilayani Bahi tarehe 14.4.2014.

No comments: