Monday, November 11, 2013

YAH:Mchango wa ununuzi wa jengo la Madrasa Buguruni Dar

Al-khayr Madrasa ilipokuwa mwanzo kabla ya kuuzwa
Al-khayr Madrasa ilipo sasa panapotakiwa kuendelezwa
Al-khayr Madrasa, iliyoanzishwa mwaka 1980, Buguruni Kisiwani jijini Dar es salaam, Tanzania, imelazimika kuhamishwa sehemu iliyokuwepo kwenda sehemu nyingine kutokana na uboreshaji wa miundombinu ya eneo hilo, mnunuzi wa Madrasa hiyo alinunua kwa Tsh. 30,000,000/= (Milioni thelathini) kutokana na udogo wa eneo.

Na nyumba ambayo imepatikana ni yenye namba ILALA/BUG/KISW/655. Ina thamani ya Shilingi 50,000,000/= (Milioni hamsini) na tayari zimeshalipwa zile Milioni Thelathini kwa makubaliano ya kumalizia deni la Milioni ishirini ifikapo Tar: 30/02/2014. Mkataba ambao umefanyika Tar:04/04 2013 . Shauri hilo limefanyika mahakama ya hakimu mkazi wa wilaya ya Ilala.

MALENGO
Uongozi wa Al-khayr Madrasa unakusudia kuanzisha kituo cha kulelea watoto yatima, chekechea pamoja na muendelezo wa Madrasa. Hivyo basi ndugu zetu waislamu na wasiokuwa waislamu tunaomba kwa kila atakae guswa na jambo hili atusaidie kwa kadri ya uwezo wake ipatikane hiyo shilingi Milioni 20 tunayodaiwa na mwenye nyumba/eneo, kama inavyoonekana pichani: kwa mawasiliano zaidi wasiliana na uongozi wa madrasa:

O713-898686-Mussa Hamadi Ally
0713-574043-Uwessu Hamidu Belege
0716-178823-Lule Ally Ibrahim

No comments: