Monday, November 04, 2013

Wambura akaimishwa-mikoba ya Angetile

Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemteua Bw. Boniface Wambura kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa TFF. Uteuzi huo ni kuanzia Novemba 2 mwaka huu.

Aidha aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah ameagizwa aende likizo ya malipo hadi atakapomaliza mkataba wake.

Kamati ya Utendaji inaviomba vilabu, vyama vya wilaya, vyama vya mikoa, vyama shiriki na wadau wote kumpa ushirikiano Bw. Boniface Wambura katika utekelezaji wa majukumu yake.
  
Jamal Malinzi, Rais TFF
 Dar es Salaam
 Novemba 3, 2013

No comments:

Makamu wa Rais Dkt. Mpango Awasili Marekani kwa Kikao cha UNGA 80

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango , leo tarehe 21 Septemba 2025 amewasili jijini New York, Marekani . ...