Wednesday, November 27, 2013

WAZIRI DK.NCHIMBI AZINDUA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITATU WA KUBORESHA MADAWATI YA KIJINSIA NA WATOTO NDANI YA JESHI LA POLISI

IMG_2363
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dr. Alberic Kacou akisalimiana na Kamanda wa Kanda Maalum Dsm, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Suleiman Kova alipowasili kwenye uzinduzi wa Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa Kuboresha Madawati ya Kijinsia na Watoto ndani ya Jeshi la Polisi. Tukio hilo lilifanyika Kituo cha Polisi Chang’ombe, Temeke jijini Dar es Salaam.
IMG_2364
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dr. Alberic Kacou akibadilishana mawazo na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema.Kulia ni Kamanda wa Kanda Maalum Dsm, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Suleiman Kova. Kushoto ni Wanamawasiliano kutoka Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Hoyce Temu na Sangita Khadka.
IMG_2370
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema akimtambulisha mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi kwa baadhi ya maafisa wa Jeshi la Polisi nchini mara baada ya kuwasilia eneo la tukio.
IMG_2374
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi akibadilishana mawazo na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema (kushoto) na Kulia ni Kamanda wa Kanda Maalum Dsm, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Suleiman Kova wakati wakielekea jukwaa kuu.
IMG_2377
Balozi wa Ireland nchini Fionnuala Gilsenan (katikati) akiteta jambo na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dr. Alberic Kacou (kushoto) Kulia ni Mkuu wa Mabalozi wa EU nchini Filiberto Sebregondi.
IMG_2381
Pichani juu na chini Maandamano yakiwasili kwenye uzinduzi wa Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa Kuboresha Madawati ya Kijinsia na Watoto ndani ya Jeshi la Polisi.
IMG_2384IMG_2385
Taasisi mbambali zikiwa zimebeba mabango yenye jumbe mbalimbali za kutokomeza ukatili wa Kijinsia.
IMG_2398
Burudani kwenye uzinduzi wa Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa Kuboresha Madawati ya Kijinsia na Watoto ndani ya Jeshi la Polisi.
IMG_2459
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akitoa hotuba yake kwa Askari na Maofisa wa Jeshi la Polisi, Viongozi wa Mashirika na Taasisi zisizo za Serikali pamoja na wakazi wa Temeke kabla ya kuzindua Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa Kuboresha Madawati ya Kijinsia na Watoto ndani ya Jeshi la Polisi. Tukio hilo lilifanyika Kituo cha Polisi Chang’ombe, Temeke jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Waziri Nchimbi akatika hotuba yake alilishukuru Jeshi la Polisi pamoja na Viongozi wa Mashirika na Taasisi zisizo za Serikali kwa kusaidia masuala ya kupambana na unyanyasaji wa kijinsia nchini.
IMG_2438
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dr. Alberic KacouIMG_2409
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema akizungumza kwenye uzinduzi wa Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa Kuboresha Madawati ya Kijinsia na Watoto ndani ya Jeshi la Polisi.
IMG_2419
Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini, Balozi Filiberto Ceriani Sebregondi akizungumza kwenye hafla hiyo.
IMG_2431
Balozi wa Ireland nchini Fionnuala Gilsenan akizungumza kwa niaba ya nchi yake ambapo amesema Ireland itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kwa ukaribu zaidi.
IMG_2460
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akizindua kitabu cha Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa kuboresha madawati ya Kijinsia na Watoto ndani ya Jeshi la Polisi katika uzinduzi uliofanyika Kituo cha Polisi Chang’ombe, Temeke jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema, wa pili kulia ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dr. Alberic Kacou, wapili kushoto ni Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini, Balozi Filiberto Ceriani Sebregondi na Kushoto ni Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova. Waziri Nchimbi akatika hotuba yake alilishukuru Jeshi la Polisi pamoja na Viongozi wa Mashirika na Taasisi zisizo za Serikali kwa kusaidia masuala ya kupambana na unyanyasaji wa kijinsia nchini
IMG_2465
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akikionyesha kitabu cha Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa kuboresha madawati ya Kijinsia na Watoto ndani ya Jeshi la Polisi katika uzinduzi uliofanyika Kituo cha Polisi Chang’ombe, Temeke jijini Dar es Salaam.
IMG_2469
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akimshukuru Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Dr. Alberic Kacou mara baada ya kuzindua Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa kuboresha madawati ya Kijinsia na Watoto ndani ya Jeshi la Polisi ulio chini ya Umoja wa Mataifa.
IMG_2471
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akikata utepe kuzindua ofisi ya Dawati la Jinsia na Watoto katika Mkoa wa Kipolisi Temeke. Kushoto ni Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini, Balozi Filiberto Ceriani Sebregondi.Waziri Nchimbi katika hotuba yake alilishukuru Jeshi la Polisi pamoja na Viongozi wa Mashirika na Taasisi zisizo za Serikali kwa kusaidia masuala ya kupambana na unyanyasaji wa kijinsia nchini.
IMG_2481
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Jeshi la Polisi pamoja na Viongozi wa Mashirika na Taasisi zisizo za Serikali baada ya waziri huyo kuzindua Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa Kuboresha Madawati ya Kijinsia na Watoto ndani ya Jeshi la Polisi. Tukio hilo lilifanyika Kituo cha Polisi Chang’ombe, Temeke jijini Dar es Salaam leo. Wapili kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema.
IMG_2486
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Dr. Alberic Kacou akiteta jambo na mmoja wa maafisa wa Jeshi la Polisi mara baada ya uzinduzi huo.
IMG_2497
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Dr. Alberic Kacou akifanya mahojiano na mwandishi wa habari wa redio wa BBC. Katikati ni Afisa Habari wa kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa Usia Nkhoma Ledama.
 IMG_2499
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akiagana na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini, Dr. Alberic Kacou mara ya uzinduzi.

No comments: