Monday, November 25, 2013

Pongezi Kutoka Kwa Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA (Mstaafu) Ananilea Nkya Kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini-Chadema Zitto Kabwe na Dr Kitila na Chadema


Aliyekua  Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA Ananilea Nkya 
----  
Vijana  Dr Kitila  na Zitto.
Nimesoma matamko yenu mliyoyatoa jana.
Nakupongezeni  maana  mmeonyesha kwamba mnatambua ninyi ni binadamu na si malaika.Mmetuonyesha sisi wananchi  kwamba ninyi ni wanasiasa wenye hofu ya Mungu. Mmetuonyesha kwamba  mmeamua kutoa maisha yenu kuwatumikia Watanzania na si kwa maslahi yenu binafsi au maslahi ya chama chenu CHADEMA pekee, bali maslahi ya Watanzania. Mmeandika historia mpya inayotoa mafunzo mbali mbali.
Ninachowashauri na hiki narejea nilichokiandika   kwenye uzi uliokuwa na tamko la Zitto ni kwamba muendelee kusimama imara na chama chenu bila kinyongo chochote kutokana na yaliyotokea  mkiwa na lengo moja  kupigania maslahi ya  umma mpana ili  NCHI YETU ISHINDE. Aidha, CHADEMA kama chama makini cha siasa, muendelee kuangalia mbele kwa umakini  sana muwashinde  wenye nia chafu dhidi yenu. Na ushindi wenu utatokana na  nia yenu safi kwa nchi yenu na watu wake, umoja wenu, umakini wenu, usafi wa matendo yenu, kuheshimiana kwenu kwenu ninyi kwa ninyi   kuonyana ili kurekebishana na kisha kusameheana kwenu.
 Siku zote mkumbuke, thawabu yenu kuu kama wanasiasa itatokana na jinsi  siasa za chama chenu  zitakavyofanikisha kuijenga Tanzania mpya isiyo na kiwango kikubwa cha rushwa kama ilivyo sasa, isiyo na ubaguzi wa haki kama ilivyo sasa kwamba  baadhi ya viongozi hata wakituhumiwa kutenda jinai kubwa mkono wa sheria hauwezi kuwadaka haraka la bda kwa shinikizo ili hali mwananchi wa kawaida akiiba hata ugali anaweza kuishia jela wiki inayofuata .   
Kadhalika Tanzania  mpya yenye hospitali nzuri zenye vifaa, madawa na madaktari  (naamini Dr Sengondo Mvungi asingekufa kama tulikuwa na hospitali nzuri hapa yenye vifaa na madawa madaktari wangemuwahi), shule nzuri na Tanzania mpya isiyo na  pengo kubwa   la kipato kati ya vwanasiasa na watumishi wengine wa umma n.k.
Nawatia shime  wote mnaopigania wananchi  na  Mungu awabariki sana.
By the way you kijana Samsoni Mwigamba sikusoma tamko lake yeye kasemaje?
 

No comments: