Thursday, November 28, 2013

Rais Jakaya Kikwete Akagua na Kuzindua Miradi Mkoa Mpya wa Simiyu

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Bwana Saguda Kasili mlemavu ambaye pia ni mtendaji wa kijiji cha Ng’wang’wali jana  wakati aliposimama kijijini hapo kuwasalimia wananchi wa eneo hilo
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la Old Maswa muda mfupi baada ya kuzindua ujenzi wa barabara ya kilometa ya Bariadi-Lamadi 71.8 huko eneo la old Maswa, Mkoani Simiyu.
 Msanii wa kundi la sanaa kutoka Bariadi akicheza na nyoka aina ya Chatu wakati wa uzinduzi wa Ujenzi wa Barabara ya Bariadi –Lamadi  Jana 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli(watatu kushoto),Mbunge wa Bariadi  Mhe. Andrew Chenge(kushoto)pamoja na viongozi wengine wakifunua kitambaa kuashiria kuweka jiwe la msingi na kuzindua ujenzi wa Barabara ya Bariadi-Lamadi yenye urefu wa kilometa 71.8 huko enelo la Old Maswa mkoa mpya wa Simiyu jana
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi Mradi wa Umeme katika kijiji cha Nkololo wilayani Bariadi, Mkoa wa Simiyu  Jana.Weninge katika picha kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mh. Steven Masele, Mbunge wa Bariadi Mhe.Andrew Chenge(wapili kushoto),Paroko wa Nkololo Padri Paulo Fegan(wanne kushoto) na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Pascal Mabiti.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya wananchi waliohudhuria ufunguzi wa Barabara ya Bariadi Lamadi jana.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli(pembeni ya Rais kulia) pamoja na viongozi wengine akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi ujenzi wa Barbara ya Bariadi Lamadi yenye urefu wa kilometa 71.8 huko eneo la Old Maswa jana.Picha na Freddy Maro-IKULU

No comments: