Wednesday, November 27, 2013

Chadema kimewaandikia barua za kuwavua rasmi nyadhifa za uongozi Zitto Kabwe na Dk Kitila Mkumbo


  
Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimesema kimewaandikia barua aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zitto Kabwe na Mjumbe wa kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo ambazo wanapaswa kujieleza kwa siku kumi na moja, kisha watapata fursa kujieleza mbele ya kamati kuu maalumu kwa nini wasifukuzwe kutoka Chamani. Akizungumza katika makao makuu ya chama hicho, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John Mnyika alisema barua hizo zipo tayari na wahusika watapatiwa wakati wowote kuanzia jana 

Mnyika alikuwa akitoa taarifa ya kikao cha Utekelezaji cha sekretarieti ya chama hicho iliyoketi baada ya mkutano wa kamati kuu iliyoketi tarehe 20 – 22 Novemba mwaka huu. Ni katika Mkutano huo, Mwanasheria Mkuu wa Chama hicho, Tundu Lissu alisema kuwa mkutano uliofanywa na Zitto na Dk Kitila mbele ya waandishi hawajazungumzia tuhuma zinazowakabili, badala yake walichofanya ni kujitungia tuhuma ambazo kimsingi sizo zilizowavua nafasi zao. 

 Lissu alisema, Zitto na Dk Kitila hawakusimamishwa nyadhifa zao kwa masuala ya PAC, Uchaguzi wa mwaka 2010, wala kutoshiriki kwenye operesheni za chama au sababu nyingine, na walitaja hizo sababu ili kupotosha tuhuma zinazowakabili kwa jamii: “walichokifanya kina Zitto na Kitilla ni "Diversion" (kubadili mwelekeo) wa mashtaka yao yanatokana na waraka wa kihaini wa mabadiliko ambao ni kinyume na katiba, kanuni na maadili na itifaki ya Chama. anawaambia waandishi, "wamevuliwa nafasi zao na kamati kuu kwa sababu ya waraka wenye nia ovu" alisema Lissu. 

Aliongeza kuwa CHADEMA kina mwongozo wa uchaguzi uliopitishwa na kamati kuu, Zitto na Kitila wanaufahamu ingawa haijulikani ni kwa nini wao walienda kinyume na mambo yanayojadiliwa katika kamati kuuu Aidha, Lissu alieleza kuwa Dk Kitilla anapotosha umma na wanachama kwa kauli yake kuwa Kamati Kuu haina mamlaka ya kumvua yeye nafasi yake ya Ujumbe wa Kamati Kuu maana amechaguliwa na Baraza Kuu. 

Alimtaka Kitila na Zitto waangalie vyema katiba ya Chama hasa majukumu ya Kamati Kuu, pale yanaporuhusu mwanachama yeyote kusimamishwa au kufutiwa uachama haraka kama Kamati Kuu itaona kuna umuhimu wa kufanya hivyo. Kigaila alisema, Kamati kuu iliyoketi Novemba 20-22/2013 ilipitisha ratiba ya uchaguzi wa ndani ya chama kama ifuatavyo:-

 .22/11/2013 - 14/12/2013 ni kukamilisha zoezi la usajili wa wanachama, 15 Desemba hadi 15 Januari uchaguzi ngazi za vitongoji, 16 hadi 30 Januari 2014 Rufaa na ukaguzi, ambapo tarehe 01 hadi 15 Februari ni uchaguzi wa matawi. 

.CHADEMA pia ilisema 16 hadi 29 Februani ni kusikiliza rufaa na ukaguzi, ambapo uchaguzi wa majimbo utaanza rasmi 1 hadi 10 Aprili, huku uchaguzi ngazi ya Wilaya ukitarajiwa kufanyika 25 Aprili hadi Mei 5 mwaka 2014, na ngazi ya Mikoa ni 20 hadi 25 Mei. 

.Uchaguzi wa kanda unatarajiwa kufanyika Julai 9, na haada ya hapo Julai 23 hadi 30 utakuwa ndiyo muda wa uchaguzi ngazi ya Taifa, utakaoanza na Baraza la Wazee, Baraza la Vijana, Baraza la Wanawake kisha Uchaguzi wa ndani ya Chama. 

*VIDEO:MakutanoShow
               ITVHabari

No comments: