Friday, November 15, 2013

TIMKA NA BODABODA YA VODACOM YAFIKIA PAZURI‏

Meneja Uhusiano wa Umma Vodacom Tanzania,Bw.Matina Nkurlu(katikati)akiwaonesha moja ya namba ya  simu ya mshindi aliejishindia Pikipiki katika promosheni ya”Timka na Bodaboda” kwa Ofisa wa huduma za ziada wa kampuni hiyo Rashid Maggid(Kushoto)na Msimamizi wa bodi ya  Michezo ya kubahatisha nchini,Bw.Emmanuel Ndaki.Wakati wakichezesha droo ya promosheni hiyo,jumla ya washindi(125)wamejishindia Pikipiki na fedha taslimu kiasi cha shilingi Milioni (70)zimenyakuliwa.Ili kujiunga na promosheni hii TUMA NENO PROMO kwenda 15544.
Meneja Uhusiano wa Umma Vodacom Tanzania,Bw.Matina Nkurlu,akisisitiza jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani)kuhusiana na umuhimu wa watanzania na wateja wa Vodacom kushiriki katika Promosheni ya ”Timka na Bodaboda”Jumla ya washindi(125)wamejishindia Pikipiki na fedha taslimu kiasi cha shilingi Milioni (70)zimenyakuliwa Wengine kushoto ni Ofisa wa huduma za ziada wa kampuni hiyo Rashid Maggid na kulia ni Msimamizi wa bodi ya  Michezo ya kubahatisha nchini,Bw. Emmanuel Ndaki.Ili kujiunga na promosheni hii TUMA NENO PROMO kwenda 15544.
Ofisa wa huduma za ziada wa Vodacom Tanzania,Bw.Rashid Maggi(kushoto)Msimamizi wa bodi ya  Michezo ya kubahatisha nchini,Bw. Emmanuel Ndaki(kulia)wakifurahia jambo wakati Meneja Uhusiano wa Umma Vodacom Tanzania Bw.Matina Nkurlu akizungumza na mmoja wa washindi wa Pikipiki katika promosheni ya”Timka na Bodaboda”inayoendeshwa na kampuni hiyo.Jumla ya washindi(125)wamejishindia Pikipiki na fedha taslimu kiasi cha shilingi Milioni (70)zimenyakuliwa.Ili kujiunga na promosheni hii TUMA NENO PROMO kwenda 15544.
Taarifa kwa vyombo vya Habari
Timka na Bodaboda ya Vodacom yafikia patamu
Bodaboda 125 na Milioni 70 tayari zimenyakuliwa
Dar es Salaam,Huku maisha ya maelfu ya Watanzania yakiendelea kuboreshwa siku hadi siku kupitia Promosheni ya “Timka na Boda Boda” inayoendeshwa na kampuni ya Vodacom Tanzania. Jumla ya Watanzania 125 wamejishindia usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda na milioni fedha taslimu Milioni 70 zikinyakuliwa.
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu, amesema siku zote Vodacom imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha inaboresha maisha ya wateja wake ambao mchango wao umeifanya kampuni hiyo kuendelea kuwa namba moja hapa nchini.
“Lengo letu sisi kama Vodacom ni kuhakikisha tunaendelea kuimarisha maisha ya wateja wetu ambao wamekuwa wakituunga mkono siku zote, Tunaamini kuwa kwa kuboresha maisha ya wateja wetu kutoka katika faida tunayoipata ili kuwawezesha wao kuendelea pia kutuunga mkono siku hadi siku na kwa nguvu zaidi,” alisema Nkurlu na kuongeza

No comments: