.jpeg)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea rasmi Ripoti ya Tume ya Rais ya Kutathmini Maboresho ya Mfumo wa Kodi nchini katika hafla iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, tarehe 18 Machi 2026.
Ripoti hiyo iliwasilishwa na Mwenyekiti wa Tume, Balozi Ombeni Sefue, ambaye alieleza kuwa mapendekezo yaliyomo yanalenga kuimarisha mfumo wa kodi ili uwe rafiki kwa wawekezaji, wenye tija kwa wananchi, na unaochochea ukuaji wa uchumi wa taifa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Samia alisisitiza umuhimu wa maboresho ya mfumo wa kodi yatakayojenga uchumi jumuishi, kuongeza uwazi na ufanisi, pamoja na kuimarisha mazingira ya biashara nchini.
Ripoti hiyo inatarajiwa kuwa chachu ya mageuzi ya sera za kodi, hatua itakayosaidia kuongeza mapato ya ndani, kuvutia uwekezaji zaidi, na kuharakisha maendeleo endelevu ya Taifa.
Serikali inaendelea kuonesha dhamira thabiti ya kuimarisha uchumi kupitia sera shirikishi zinazoweka mbele maslahi ya wananchi, huku ikiendeleza juhudi za diplomasia ya kiuchumi ili kufungua fursa mpya za maendeleo.
#KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiplomasiaYaKiuchumi






No comments:
Post a Comment