Saturday, January 23, 2016

WAWILI WAPOTEZA MAISHA NA WENGINE 43 KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA BASI LA BM MKOANI MOROGORO


Basi la Kampuni ya BM linalofanya safari zake kati ya Dar es salaam - Morogoro, limepata ajali usiku wa kuamkia leo katika eneo la Mikese Mkoani Morogoro, na kupelekea watu wawili kupoteza maisha na wengine 43 kujeruhiwa. Basi hilo liligongana na gari lingine na kutumbukia kwenye Korongo.
Chanzo cha ajali hiyo, inadaiwa ni mwendo kasi wa Basi hilo uliopelekea kushindwa kusimama baada ya kukuta Lori lililokuwa limeharibika na kuegeshwa pembeni, huku upande mwingine kukiwa na Lori lingine likipita.
Basi la Kampuni ya BM linavyoonekana baada ya kupata ajali hiyo.

No comments:

Waziri Kombo akutana na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Umoja wa Afrika

   Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo amekutana na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa U...