Thursday, January 14, 2016

NAIBU WAZIRI WIZARA YA HABARI AFANYA ZIARA RUFIJI PWANI

wan2Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Mh. Anastazia Wambura wa pili kutoka kulia akipokea taarifa ya utekelezaji wa  kikundi cha Sanaa za maigizo kilichopo wilaya ya Rufiji Bw. Bashiru Kibopo wakati ya ziara ya kujionea shughuli za maendeleo ya sekta ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Wilayani humo,wa pili kutoka kushoto ni Mbunge wa jimbo hilo Mh. Allyseif Ungando na wa kwanza kulia ni Katibu Tawala Wilaya ya Rufiji Bi. Maria Katemana. (Picha na Benjamin Sawe- WHUSM)
wan3
Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Mh. Anastazia Wambura aliyenyoosha mkono akiongea na baadhi ya wasanii waliojenga katika kijiji cha Wasanii na wanahabari kilichopo  Wilayani Mkuranga  wakati ya ziara aliyofanya ya kujionea shughuli za maendeleo ya sekta ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Wilayani humo. (Picha na Benjamin Sawe- WHUSM)
wan4
wan5
Mbunge wa jimbo la Mkuranga Mh. Abdalla Ulege akiongea na wakazi wa jimbo lake wakati wa ziara ya Naibu Waziri, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura ya kujionea shuguli za maendeleo ya sekta hiyo. (Picha na Benjamin Sawe- WHUSM)
wan6
Mwenyekiti wa mtandao wa wasanii (SHIWATA) Bw. Cassim Talib katikati akimuonyesha baadhi ya nyumba za wasanii na wanahabari zilizopo Wilayani humo Mh. Anastazia Wambura wa kwanza kushoto wakati ya ziara ya kujionea shughuli za maendeleo ya sekta ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Wilayani humo., kulia ni msanii wa sanaa za maigizo maarufu kama mzee Chilo. (Picha na Benjamin Sawe- WHUSM)
wan7
Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura akisalimiana na Mbunge wa Rufiji Mh. Allyseifu Ungando wakati wa ziara ya kujionea maendeleo ya sekta ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wilayani humo. (Picha na Benjamin Sawe- WHUSM)

No comments: