Friday, January 23, 2015

WhatsApp yawabana watumiaji

Mtandao wa kijamii wa WhatsApp unawabana watu wanaotumia huduma hio kupitia programu bandia na ambayo haijaidhinishwa ya Android kwa muda wa saa 24.
WhatsApp ambayo inamilikiwa na Facebook, ilisema kuwa imechukua hatua dhidi ya watumiaji wa huduma ya WhatsApp Plus kwa sababu ya wasiwasi kwamba programu hiiyo huenda iksababisha kuvuja kwa taarifa za siri za watumiaji wa WhatsApp.
Programu hio bandia na isio rasmi ya Android inawezesha watumiaji wa WhatsApp Plus kupamba mawasiliano yao wanavyotaka.
Wataalamu wanasema kwamba watumiaji wa Android wanapaswa kuwa makini na kutahadhari kuhusu wanavyodownload programu flani au 'Apps'.
Mtandao wa WhatsApp ulisema hivi karibuni kwamba ina watumiaji milioni 700 wanaotuma ujumbe bilioni 30 kila siku. Kwa sasa inatoza dola 0.99 kwa watumiaji wake wanaotumia huduma ya WhatsApp Plus kila mwaka.
''Lengo letu ni kuhakikisha kwamba huduma ya WhatsApp ni ya kasi kwa wanaoitumia, hilo ndio jambo muhimu sana kwetu,'' alisema msemaji wa kampuni hio.
''Watu wengine wamebuni progarmu ambazo bado hazijaidhinishwa na sasa wanazitumia na WhatsApp , kitu ambacho kinaweza kusababisha kupotea kwa ujumbe au baadhi ya taarifa kuvujishwa. ''
''Bila shaka jambo hili linakwenda kinyume na malengo yetu ya kutoa huduma kwa wateja wetu. Kuanzia leo tutaanza kuchukua hatua kali dhidi ya wanaotumia programu ambazo hazijaithinishwa ili kuweza kutumia programu zetu na pia kuwatahadharisha wanaozitumia programu hizo''.
Kulingana na moja ya maduka ya kuuza programu za kwenye mitandao, programu ya WhatsApp Plus yenyewe ilikuwa imekuwa dowloaded mara milioni 35

No comments: