Tuesday, January 27, 2015

DKT. FENNELA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAAFISA MAWASILIANO SERIKALINI NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI

2
2- Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akiwaeleza jambo Maafisa Mawasiliano Serikalini kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara. Katika kikao kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini Januari 26, 2015 Mjini Mtwara
Picha zote na Hassan Silayo
3
 Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi wa kikao kazi hicho Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara.
4
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akiwaeleza washiriki wa Mkutano huo umuhimu wa kuelimisha umma kuelekea upigaji kura ya maoni na kuwataka wahariri wa vyombo vya habari nchini kuwa mstari wa mbele katika kutekeleza suala hili la kitaifa.
5
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya JL Communication inayochapisha magazeti ya Jambo leo na StaaSpoti Bw. Theophil Makunga akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara pia aliwataka Maafisa Mawasiliano kutengeneza mazingira yatayowezesha kufanya kazi na wanahabari.
8
8- Mhadhiri wa Chuo kikuu cha Tiba na Sayansi Shirikishi(MUHAS) Dkt.Ave Maria Semakafu akimueleza jambo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara(mwenyekoti jekundu) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Sihaba Nkinga.
9
Katibu wa Jukwaa la Wahariri akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga wakati wa kikao kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini leo Mjini Mtwara.
10
 Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini(TAGCO) Bw. Innocent Mungy akiwasilisha Mada kwa washiriki wa Mkutano huo kuhusu wajibu wa Maafisa Mawasiliano Serikalini katika kuimarisha mawasiliano ya serikali kwa umma.
11
Mjumbe wa Jukwaa la wahariri Bw. Salim Salim akiwaeleza washiriki wa mkutano huo Umuhimu wa kuwa na Usiri katika utendaji kazi.
…………………………………………………………………………….
Na Frank Mvungi-MAELEZO
Serikali imevitaka vyombo vya Habari nchini kuwaelimisha wananchi kuhusu Katiba inayopendekezwa ili waweze kujitokeza kwa wingi kuipigia kura
Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari Vijana utamaduni na Michezo Mh.Dkt Fenella Mukangara wakati wa akifungua kikao Kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinachofanyika Mkoani Mtwara.
Akifafanua Mh.Dkt Mukangara amewataka Maafisa Mawasiliano Kushirikiana na vyombo vya habari katika kuuelimisha umma kuhusu Katiba nayopendekezwa ili wananchi waweze kufanya uamuzi sahihi wakati wa kupiga kura ya maoni.
Akizungumzia swala la wananchi kujiandisha ili wapate fursa ya kupiga kura ya maoni Dkt Mukangara amesema ni vyema Maafisa Mawasiliano wakashirikiana na vyombo vya habari kuwahamasisha wananchi kujiandisha kwa wakati muafaka.
Pia Waziri Mukangara alisisitiza kuwa Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuimarisha uhuru wa wajibu wa vyombo vya habari pamoja na wajibu wa Maofisa Mawasiliano kutoa taarifa kwa umma ndio maana imeandaa kikao kazi hicho.
Aidha Dkt. Fenella alisema kuwa ushirikiano kati ya Maafisa Mawasiliano Serikalini na Wahariri wa vyombo vya habari hapa nchini utasaidia kutafuta namna bora ya kutoa habari kwa umma na kwa usahihi na weledi unaohitajika.
Kikao Kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinafanyika Mkoani Mtwara kuanzia Januari 26,hadi februari Mosi 2015 katika ukumbi wa NAF Hotel Mkoani Mtwara kikiwashirikisha wahariri wa vyombo kutoka vyombo mbalimbali vya Habari hapa nchini.

No comments: