Friday, January 23, 2015

WAZIRI CHIKAWE AWAAPISHA WAJUMBE WA SEKRETARIETI YA TUME YA JESHI LA POLISI NA MAGEREZA DAR ES SALAAM

unnamed (16)
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia-meza kuu) akiongoza kikao cha Tume ya Jeshi la Polisi na Magereza inayoshughulikia masuala ya kiutumishi na kiutendaji wa askari katika Majeshi hayo, katika Ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dar es Salaam jana. Kushoto Meza Kuu ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Pereira Ame Silima. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
unnamed (14)Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akimuapisha Afisa wa Jeshi la Magereza, Elmas Linus Mgimwa kuwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Jeshi la Polisi na Magereza inayoshughulikia masuala ya Utumishi na Utendaji wa askari wa majeshi hayo, katika Ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam jana. Kulia kwa Waziri Chikawe ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima, na katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
unnamed (15)Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akimpa hati ya kiapo Afisa Utumishi wa wizara hiyo, Ernest Maalugu kuwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Jeshi la Polisi na Magereza inayoshughulikia masuala ya Utumishi na Utendaji wa askari wa majeshi hayo, katika Ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima, na kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments: