Tuesday, January 20, 2015

ARSENAL FC YATEMBELEA PSPF KWA LENGO LA KUSAKA FURSA ZA MAHUSIANO YA KIBIASHARA


Mkurugenzi wa Mahusiano ya kimaendeleo wa Klabu ya Arsenal Bw. Sam Stone (Kulia) akimkabidhi jezi ya timu hiyo Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Adam Mayingu. Kushoto ni Bw. Daniel Willey, Meneja wa Mahusiano ya Kimaendeleo ya Arsenal. Maafisa hao wapo nchini kwa lengo la kukutana na wadau mbalimbali ili kufungua mahusiano ya kibiashara, katika mpango huo makocha wa timu hiyo na baadhi ya nyota waliowahi kuchezea timu hiyo watapata fursa kutembelea Tanzania. Klabu ya Arsenal ni kati ya klabu maarufu ulimwenguni ambayo inashiriki ligi maarufu duniani ya Barclays.
Mkurgenzu Mkuu wa PSPF Bw. Adam Mayingu (kushoto) akimkabidhi zawadi Afisa Mtendaji Mkuu wa EAG Group, Bw Imani Kajura ambaye ni mwenyeji wa maafisa kutoka klabu ya Arsenal ambao wapo nchini kwa ajili ya kukutana na wadau mbalimbali kwa lengo kufungua mahusiano ya kibiashara.

No comments: