Tuesday, September 08, 2015

MABWAWA YA MAJI TAKA ENEO LA VINGUNGUTI KUANZA KUZALISHA GESI.


 Mratibu wa Mradi wa kuzalisha gesi ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa 4 katika fani ya Uhandisi wa Mazingira, Chuo Kikuu cha Ardhi John Rutahirwa Akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu moja ya mtambo wa kukusanyia maji taka kutoka majumbani eneo la mradi wa kuzalisha gesi Vingunguti.Gesi hiyo itaanza kutumika mwezi Desemba mwaka huu.
 Meneja Uhusiano wa DAWASCO Bi.Neli Msuya (kulia) akiwa na Mtaalam anayehusika na ujenzi, mafunzo na usimamizi wa mfumo wa mradi wa kuzalisha Gesi Vingunguti ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa nne wa shahada ya Uhandisi wa Mazingira, Chuo Kikuu cha Ardhi Rukia Yange wakionyesha moja ya kifungashio cha Gesi itakayotumika majumbani Kutokana na maji taka yanayokusanywa eneo la Vingunguti.Mradi huo unalenga kuwapunguzia  wananchi gharama za uhifadhi wa maji taka na kuwapatia nishati ya gesi kwa gharama nafuu itakayowasaidia kuondokana na matumizi ya mkaa.
 Jumanne Saidi Fundi ujenzi wa vyoo na msimamizi wa mradi wa majaribio wa Biogasi Vingunguti akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu kazi ya ufungaji wa miundombinu ya kuzalisha gesi katika eneo la Vingunguti.
 Mtaalam anayehusika na ujenzi, mafunzo na usimamizi wa mfumo wa mradi wa kuzalisha Gesi Vingunguti ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa nne wa shahada ya Uhandisi wa Mazingira, Chuo Kikuu cha Ardhi Rukia Yange akitoa maelezo kwa waandishi wa habari kuhusu maji taka yanayokusanywa eneo la Vingunguti ambayo yatazalisha nishati ya Gesi na kuwahudumia wanaoishi kuzunguka mabwawa ya Maji Taka Vingunguti.

No comments: