Thursday, June 11, 2015

DKT.MAGUFULI AZIDI KUPATA WADHAMINI MIKOA YA KAGERA, MARA NA MWANZA


Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Chato Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikabidhiwa fomu yenye orodha ya Wadhamini waliojitokeza kumdhamini katika mbio za kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano kupitia chama hicho kutoka kwa Katibu wa CCM Wilayani Musoma.
Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Chato Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikabidhiwa fomu yenye orodha ya Wadhamini waliojitokeza kumdhamini katika mbio za kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano kupitia chama hicho kutoka kwa Katibu wa CCM Wilayani Kagera.
Zoezi la udhamini katika wilaya ya Magu likiendelea huku Waziri wa Ujenzi Dkt. Magufuli akifatilia kwa makini.
Waziri wa Ujenzi Dkt. Magufuli akisalimiana na baadhi ya wadhamini wake waliojitokeza Wilayani Magu kwa ajili ya kumdhamini.
Zoezi la udhamini katika wilaya ya Musoma mkoani Mara likiendelea.
Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Chato Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wadhamini wake Wilayani Musoma mara baada ya kukabidhiwa fomu zake kutoka kwa katibu wa CCM Wilaya ya Musoma.
Waziri wa Ujenzi Dkt. Magufuli wakwanza kulia akisaini kitabu katika Ofisi Kuu za CCM Mkoani Mwanza.
Waziri wa Ujenzi Dkt. Magufuli akisalimiana na baadhi ya Wanachama wa CCM waliojitokeza kumdhamini Mkoani Kagera.

No comments:

KUSANYENI KODI NA MADENI BILA KUOGOPA MTU YEYOTE– WAZIRI AKWILAPO ASEMA AKIZINDUA BODI MPYA YA NHC

  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Leonard Akwilapo, akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),...