Wednesday, June 17, 2015

ZIARA YA WAZIRI WA ARDHI LUKUVI MKOANI LINDI

 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh William Lukuvi akisalimiana na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi mara baada ya kuwasili mkoani humo kwa ziara ya siku mbili amapo atasikiliza na kutatua migogoro ya ardhi katika maeneo mbalimbali yenye migogoro katika mkoa huo.
 Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mama Mwantum Mahiza akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo katika mkoa huo kwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mh William Lukuvi mara baada ya Waziri Lukuvi kuwasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh William Lukuvi akijadiliana jambo na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mama Mwantum Mahiza muda mfupi baada ya Mama Mahiza kutoa taarifu fupi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh William Lukuvi akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa shirika la nyumba la Taifa Mkoa wa Lindi Bw Mussa Patric Kamenda badaa ya mkurugenzi huyo kutoa taarifa kwa Mheshimiwa Waziri jinsi shirika hilo linanvyotekeleza miradi mbalimbali katika mkoa huo.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh William Lukuvi (kulia) akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mama Mwantum Mahiza (kushoto) kuhusu ujenzi wa nyumba unaofanywa na Shirika la nyumba la Taifa mkoani Lindi. Katikati ni mfanyabiashara wa mkoa wa Lindi Bw Kassim Abdallah ambaye amenunua mojawapo nyumba ambazo zimejengwa na shirika la nyumba la Taifa.
Waziri wa ArdhiNyumba na Maendeleo ya Makazi Mh William Lukuvi akitoa malelekezo kwa Bwana Mussa Patric Kamenda Mkurugenzi wa shirika la nyumba la Taifa Mkoa wa Lindi   namna bora ya kutumia viwanja kwa ujenzi wenye manufaa kwa kulunufaisha shirika hilo.
Picha na Clarence Nanyaro.

No comments: