Thursday, June 25, 2015

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, LAZARO NYALANDU APATA WADHAMINI MKOANI RUVUMA

2
 WANACHAMA na mashabiki wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Ruvuma, wakishangilia kwa furaha wakati Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akiwasili kwenye Ofisi za CCM Mkoa wa Ruvuma, kuomba udhamini katika harakati zake za kuwania kuteuliwa kuwania urais kupitia CCM.
3
 WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akizungumza na wanachama wa CCM waliojitokeza kumdhamini katika harakati zake za kuwania kuteuliwa na Chama kugombea urais kwenye uchaguzi mkuu ujao.
4
 WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akikabidhiwa fomu za udhamini na Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma, Verena Shumbusho, baada ya kudhaminiwa na zaidi ya wanachama 90.
5
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akipokewa na mamia ya wanachama, mashabiki na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alipowasili mkoani Ruvuma jana, kuomba udhamini katika harakati zake za kuwania kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM katika nafasi ya urais.
689

No comments:

WAZIRI WA FEDHA: BAJETI YA 2026/27 KUIJENGA TANZANIA YA DIRA YA 2050

  Na Eva Valerian, WF, Dodoma Serikali imesema Bajeti Kuu ya mwaka wa fedha 2026/27 ni ya kipekee kwa kuwa ndiyo bajeti ya kwanza itakayot...