Tuesday, June 30, 2015

KINANA ZIARANI UKEREWE

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwapungia wakazi wa kijiji cha Sambi kata ya Irugwa, wilayani Ukerewe waliojitokeza kwa wingi kumpokea ,Kinana ameweka historia kwa kuwa kiongozi wa kwanza kufika katika kisiwa hicho akiwa kwenye ziara ya kukagua, kuhimiza na kusimamia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi pamoja na kukagua uhai wa Chama.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimina na mmoja wa wakazi wa kata ya Irugwa
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kijiji cha Sambi kata ya Irugwa.
 Wananchi wa Kata ya Irugwa wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (katikati) akiwapingia mkono wananchi waliojitokeza kumpokea kwenye kisiwa cha Ukara.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifuturu ndani ya meli ya Mv.Nyerere akiwa njiani kuelekea Nansio Ukerewe, Wengine pichani ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza Mhe. Antony Diallo (katikati) na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Magessa Mulongo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimu wakazi wa Nansio waliojitokeza kwa wingi kumpokea.
(Picha na Adam Mzee)

No comments:

DKT. ABBASI AKAGUA MIRADI YA UTALII PORI LA AKIBA LA PANDE, ATOA MAAGIZO YA KUKAMILIKA KABLA YA AFCON 2027

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, leo Julai 23, 2026, ametembelea Pori la Akiba la Pande jijini Dar es Salaa...