Wednesday, June 24, 2015

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA LEO ALIKUWA NA WANAKWIMBA

????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Mbunge wa jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor wakati alipowasili katika kijiji cha Hungumalwa njia panda ya Mwamashimba wakati alipoanza ziara katika jimbo hilo akitokea jimbo la Misungwi mkoani Mwanza, Kinana yuko katika ziara ya kikazi ya mkoa wa Mwanza yenye lengo la kukagua Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010-2915 inayotekelezwa na serikali huku akisikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuzipatia ufumbuzi na kuhimiza uhai wa Chama cha Mapinduzi, Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-KWIMBA)
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM wakipokelewa na Sungusungu walinzi wa asili wa kabila la kisumuka wakati alipowasili katika kijiji cha Hungumalwa wilayani Kwimba.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amevishwa mavazi ya Sungusungu huku akiimbiwa nyimbo na sungusungu hao wakati alipowasili katika kijiji cha Hungumalwa.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katikati akiongozana na Mbunge wa jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor kulia ni Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza Ndugu Miraji Mtaturu wakati alipowasili kukagua mradi wa ujenzi wa zahanati ya Hungumalwa.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua kikundi cha ngoma mara baada ya kuwasili katika zahanati ya Hungumalwa ambapo alikagua ujenzi wake.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza katika zahanati ya Hungumalwa ambayo ujenzi wake unaendelea katikati ni kijana mdogo Diwaniwa wa Hungumalwa Shija Marando ambaye amesimamia ipasavyo ujenzi wa zahanati hiyo na kulia ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM.
????????????????????????????????????
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Ndugu Magesa Mulongo akishiriki ujenzi wa zahanati ya Hungumalwa mara baada ya Katibu Mkuu wa CCM kukagua ujenzi wake kushoto ni Mbunge wa jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kulia , Mkuu wa mkoa wa Mwanza Ndugu Magesa Mulongo na Mbunge wa jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor kulia wakipanda mbegu za miti wakati Kinana alipotembelea kikundi cha utunzaji wa mazingira cha Ngudu wilayani Kwimba.
????????????????????????????????????
Mbunge wa jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama wakati Katibu Mkuu wa CCM alipotembelea moja ya vituo vya maji safi na salama katika mji Ngudu.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaini kitabu cha wageni wakati alipokagua majengo ya wagonjwa mahututi ICU na wodi ya wagonjwa daraja la pili katika hospitali ya wilaya ya Kwimba katika mji wa Ngudu mkoani Mwanza.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM wakiondoka hospitalinia hapo mara baada ya kutembelea hospitali hiyo na kuona huduma mbalimbali na katika hospitali hiyo.
????????????????????????????????????
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM akiwahutubia wananchi wa Ngudu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa mpira Ngudu.
????????????????????????????????????
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM akisisitiza jambo wakati akiwahutubia wananchi wa Ngudu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa mpira Ngudu.
????????????????????????????????????
Umati wa wananchi waliojitokeza katika mkutano huo kwenye uwanja wa mpira wa Ngudu wilayani Kwimba.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa mjini Ngudu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa mpira wa Ngudu.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati akiwahutubia wananchi wa mjini Ngudu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa mpira wa Ngudu.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi za waliokuwa wananchama wa Chama cha CHADEMA mara baada ya wananchi hao kujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimkabidhi kadi ya uanachama wa CCM aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA kijiji cha Ilula kata ya Ilula wilayani Kwimba Bw. Hamala Matelemki katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa mpira wa Ngudu.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi baiskeli kwa walemavu zilizotolewa na mbunge wa jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  na Mbunge wa jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor wakikabidhi vyerehani kwa vikundi vya akina mama washonaji wa nguo baada ya mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa mpira mjini Ngudu.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano huo.

No comments: