Friday, June 19, 2015

MAMIA WAFURIKA BANDA LA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA (NHIF), KUPIMA AFYA ZAO KATIKA MAONYESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR

Ofisa Uratibu na Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Genoveva Vicent (kulia), akimuelekeza jambo mwananchi aliyetembelea banda la NHIF katika maonyesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea viwanja vya Manazi Mmoja Dar es Salaam jana. Wengine wa pili kushoto ni Ofisa wa NHIF, Ambrose Manyanda na Ofisa Mawasiliano wa NHIF, Luhende Singu.
Ofisa wa NHIF, Ambrose Manyanda (kulia), akimuelekeza jambo mwananchi aliyetembelea banda la NHIF.
Mtaalamu wa Maabara wa Hospitali ya Amana, Johnbosco Kishebuka (kushoto), akimpima urefu mwananchi aliyefika katika banda la NHIF kabla ya kufanyiwa vipimo vingine.
Mwanahabari Beatrice Mbwambo (kulia), ni miongoni mwa wananchi waliojitokeza kupima afya yake katika banda la NHIF ambapo huduma hiyo ya kupima ugonjwa wa kisukari, shinikizo la damu na , saratani ya matiti.
Ofisa wa NHIF (kushoto), akitoa maelekezo kwa wananchi waliofika kwenye banda la NHIF.
Ofisa Mawasiliano wa NHIF, Luhende Singu (katikati), akiwakaribisha wananchi waliotembelea banda la NHIF.
Wananchi waliotembelea banda la NHIF wakipata maelezo mbalimbali kutoka kwa maofisa wa NHIF.
Wananchi wakiwa wamefurika banda la NHIF kwa ajili ya kupata huduma za kupima afya zao.
Wadau mbalimbali wakisubiri kupata vipimo katika banda la NHIF. 

No comments: