Wednesday, May 11, 2016

WATEJA WA “RAHISI INAYOWEZESHWA NA ACCESSMOBILE” KUTOKA ACCESSBANK KUNUFAIKA KWA ZAWADI MBALIMBALI

Pichani (kushoto) ni mmoja wa wateja ambao wamewahi kujishindia zawadi ya simu mpya na ya kisasa aina ya Huawei P8 kwa kufanya miamala mingi zaidi kupitia huduma maridhawa ya “RAHISI inayoweshwa na AccessMobile.

Mr Amos Masunga (mmoja wa wateja ambao wamewahi kujishindia zawadi ya simu mpya na ya kisasa), akipongezwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa AccessBank Tanzania, Mr. Roland Coulon.

Akitoa maoni juu ya hili, Meneja Masoko wa AccessBank, Bw. Muganyizi Bisheko, alisema kuwa, “inafurahisha sana kuona huduma hii inafanya vizuri na imeweza kukidhi kisawa sawa mahitaji ya wateja. tutaendelea kuwaweka wateja wetu mbele na kuwazadia kwa uzalendo wao na uaminifu wao katika kutumia huduma zetu.”
“Ningependa kuwashauri wateja waendelee kutumia mfumo wetu wa bure wa huduma za kibenki kwa njia ya simu, wafanye miamala mingi na wawashauri ndugu na jamaa kujiunga na mfumo huu kwa kutembelea tawi lolote la AccessBank huu ili nao waweze kufurahia miamala ya bure na kufuzu kwenye mfumo huu wa zawadi.”
Mnamo 1/5/2015 AccessBank ilizindua huduma maridhawa ya “RAHISI inayowezeshwa na AccessMobile”, huduma inayomuwezesha mteja kupata huduma zote za kibenki bure kupitia simu ya mkononi  kama ifuatavyo;
·         kupata akaunti Bure isiyo na gharama za uendeshaji
·         kuweka na kutoa fedha Bure kwenye tawi lolote la AccessBank
·        Kuhamisha Fedha Bure: Kwenda Akaunti ya Benki/M-pesa/Airtel Money/Tigo Pesa.
·                    ·        Kulipia Bili Bure: Luku/Dawasco/DSTV na nyinginezo.
            ·        Kupata taarifa za akaunti Bure: Kujua salio, kupata taarifa fupi.
·                     ·        Kuongeza salio Bure: Vodacom/Airtel/Tigo/Zantel.

Ili kujiunga na huduma hii mteja anatakiwa kutembelea tawi lolote la AccessBank lililo karibu nae na kisha atakua anapiga * 150*43# kufurahia huduma mbalimbali za Bure za kibenki mahali popote kupitia simu ya mkononi. Kwa maelezo zaidi mteja anaweza kupiga; 0659 074000, 0784 108500


AccessBank Tanzania ni Taasisi ya Kifedha inayolenga kutoa huduma za kibenki kwa wajasiriamali wadogo na wa kati. kupitia wanahisa wake wa kimataifa amabao ni AccessHolding, International Finance Corporation (Word Bank), KfW, African Development Bank na MicroVest, maono ya benki ni kujidhatiti katika uanzishaji wa mifumo ya kifedha unayochochea maendeleo ya jamii kwa kutoa huduma zilizobora kwa watu wote. 

AccessBank yaendelea kuwakumbusha wateja kuweka fedha kwenye akaunti zao za”RAHISI inayowezeshwa na AccessMobile” na kisha wafanye miamala mingi ili waokoe muda na pesa zao.Sambamba na hilo, pindi mteja afanyapo miamala mingi, unaweza kujishindia simu mpya ya kisasa”brand new smart phone”.

No comments: