Tuesday, May 03, 2016

LAPF YAKABIDHI MADAWATI YA SHILINGI MILIONI KUMI KWA MKUU WA WILAYA YA KINONDONI

JAMES1Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Salum Ally Hapi (wa pili kushoto) akimshukuru Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF James Mlowe mara baada ya kupokea msaada wa madawati 124 kwa ajili ya Shule ya Msingi Nakasangwe iliyopo Kata ya Wazo. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana.  Kulia ni Ofisa Elimu Msingi Wilaya ya Kinondoni, Kiduma Mageni.
JAMES2Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mh. Salum Ally Hapi (kulia) akipokea msaada wa madawati 124 kutoka kwa Meneja Masoko na Mawasiliano wa mfuko wa pensheni wa LAPF, James Mlowe kwa ajili ya shule za Serikali Manispaa ya Kinondoni. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Katikati ni Ofisa Elimu Msingi  Wilaya ya Kinondoni, Kiduma Mageni. 
JAMES3
Mkuu wa Wilayaya Kinondoni, Salum  Ally Hapi akizungumza katika hafla ya kupokea madawati 124 yaliyotolewa na Mfuko wa Pensheni wa LAPF jijini Dar es Salaam jana.
JAMES4Kaimu Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa  LAPF Kanda ya Dar es Salaam, Bw. Yesaya Mwakifulefule akizungumza katika hafla hiyo.
JAMES5Meneja Masoko na Mawasiliano wa  Mfuko wa Pensheni wa LAPF, Bw. James Mlowe akizungumza katika hafla hiyo.

No comments: