Thursday, May 26, 2016

ESRF YAFANYA WARSHA KUJADILI MPANGO WA MAENDELEO ENDELEVU (SDG)

DSC_2311
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akitoa neno la ufunguzi katika warsa iliyoandaliwa na ESRF ili kuzungumzia Mpango wa Mendeleo Endelevu (SDG). (Picha zote na Rabi Hume, Modewjiblog)
DSC_2313
DSC_2330
Baadhi ya washiriki waliohudhuria warsha hiyo wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii, Dkt. Tausi Kida wakati akifungua warsha hiyo.
DSC_2341
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Awa Dabo akitoa neno kwa niaba ya UNDP ambao ndiyo wasimamizi wa mpango huo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida na Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha
DSC_2354
Mgeni rasmi katika warsha hiyo, Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha akifungua warsha hiyo iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF).
DSC_2367
DSC_2384
Washiriki wakiendelea kufatilia kinachoendelea katika warsha hiyo.
DSC_2478
Stephen Chacha kutoka Shirika la Beyond 2015 for Africa akizungumza jinsi Mpango wa SDG unaweza kufanyika nchini.
DSC_2481
DSC_2521
Mmoja wa washiriki, Dkt. Kitila Mkumbo akichangia mada zilizokuwa zikijadiliwa.
DSC_2457
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Katika kusaidia kukamilika kwa Mpango wa Maendeleo Endelevu ambao unataraji kumalizika 2030, Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) imefanya warsha ambayo imekutanisha wadau mbalimbali ili kuona ni jinsi gani wanaweza kubadilishana mawazo ili kufanikisha mpango huo nchini.
Mgeni rasmi katika warsha hiyo alikuwa ni Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha ambaye wakati akifungua warsha hiyo alisema kuwa mpango huo ni muhiu wa nchi yetu kwa sababu unakwenda kubadili maisha ya kila Mtanzania ili kuondokana na umaskini na kuwa katika maisha bora kama jinsi malengo 17 ya mpango huo yanavyojieleza.
Mo Dewji Blog ilipata nafasi ya kuhudhuria mkutano huo na kukuandalia habaroi picha jinsi warsha hivyo ilivyofanyika katika ukumbi wa ESRF.

No comments: