Wednesday, May 25, 2016

YANGA YATWAA KOMBE LA SHIRIKISHO UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR


Mshambuliaji wa Timu ya Yanga, Amis Tambwe akishangilia bao la kuongoza aliloipatia timu yake dhidi ya Azam FC , katika mchezo unaopigwa hivi sasa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, ikiwa ni Fainali ya Mashindano ya Kombe la Shirikisho (ASFA). hadi Timu ya Globu ya Jamii inaingia mitamboni, Yanga wanaongoza kwa Bao 3-1. Picha na Othman Michuzi.

Kiungo Mshambuliaji wa timu ya Azam FC, Ramadhan Singano "Messi" akiichambua ngome ya Timu ya Yanga, katika mchezo unaopigwa hivi sasa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, ikiwa ni Fainali ya Mashindano ya Kombe la Shirikisho (ASFA). hadi Timu ya Globu ya Jamii inaingia mitamboni, Yanga wanaongoza kwa Bao 3-1.
 Mchezaji wa timu ya Yanga Oscar Joshua akimzuia mchezaji wa timu ya Azam FC Himid Mao kwenye mchezo wao wa Fainali ya Mashindano ya Kombe la Shirikisho (ASFA) unaochezwa jioni hii uwanja wa Taifa jijini Dar. hadi Timu ya Globu ya Jamii inaingia mitamboni, Yanga walikuwa wanaongoza Bao 3-1.
Lango la Azam  FC likiwa hatarini kuvunjwa. 

No comments: