Thursday, May 05, 2016

WAFANYAKAZI WA NHC WAPANDA MITI KATIKA MAKAZI YALIYOUZWA WANANCHI KIBADA NHC

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii, Susani Omari akizungumza na Mameneja wa NHC na Wakurugenzi wakati wa zoezi la kupanda miti katika Estate ya Kibada ikiwa ni jitihada za NHC kuboresha mazingira ya eneo hilo linalokaliwa na wakazi takribani 1,000 katika nyumba zipatazo 218 za gharama nafuu. EMT wote(Directors, Regional Managers &  Line Managers) pia wametembelea miradi ya Kawe, Morocco Square, Victoria Place, Eco Residence na Kibada ambako kumefanyika shughuli hiyo ya upandaji miti.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Shirika la Nyumba la Taifa, James Rhombo akipanda mti wa mchikichi katika eneo la makazi la NHC Kibada Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi (TAMICO), Lilian Reuben na Meneja wa NHC, Mtwara, Joseph John wakipanda mti katika eneo la makazi la NHC Kibada Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate.
Zoezi la kupanda miti likiendelea katika eneo la makazi la NHC Kibada Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate.

 Mandhari ya kupendeza ya nyumba za makazi za  NHC Kibada Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate inavyoonekana mchana huu, hizo ni barabara, mataa na mitaro ya nyumba hizo zinavyoonekana leo hii.
 Mandhari ya kupendeza ya nyumba za makazi za  NHC Kibada Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate inavyoonekana mchana huu, hizo ni barabara, mataa na mitaro ya nyumba hizo zinavyoonekana leo hii.
Wajumbe wa ziara hiyo wakisikiliza kwa makini maenelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa Shirika la Nyumba la Taifa, NHC, Haikamen Mlekio wakati wajumbe hao walipotembelea eneo hilo la makazi.
 Mandhari ya kupendeza ya nyumba za makazi za  NHC Kibada Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate inavyoonekana mchana huu, hizo ni barabara, mataa na mitaro ya nyumba hizo zinavyoonekana leo hii.
 Mandhari ya kupendeza ya nyumba za makazi za  NHC Kibada Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate inavyoonekana mchana huu, hizo ni barabara, mataa na mitaro ya nyumba hizo zinavyoonekana leo hii.
 Majengo ya kisasa ya Mradi wa NHC wa makazi wa 711 Kawe unavyoonekana kwa sasa, mradi huu ni mmoja wa miradi iliyotembeleewa na Mameneja wa Shirika la Nyumba la Taifa 
  Majengo ya kisasa ya Mradi wa NHC wa makazi wa 711 Kawe unavyoonekana kwa sasa, mradi huu ni mmoja wa miradi iliyotembeleewa na Mameneja wa Shirika la Nyumba la Taifa 
 Meneja wa NHC wa Mradi wa 711, Sawel Metili akitoa maelezo kwa mameneja wa NHC kwenye eneo la  Majengo ya kisasa ya Mradi wa NHC wa makazi wa 711 Kawe. 
  Meneja wa NHC wa Mradi wa 711, Sawel Metili akitoa maelezo kwa mameneja wa NHC kwenye eneo la  Majengo ya kisasa ya Mradi wa NHC wa makazi wa 711 Kawe. 
Wajumbe wa Menejimenti ya NHC wakiwasili katika eneo la mradi wa NHC wa 711 Kawe leo wakati walipofanya ziara katika miradi hiyo kwa lengo la kufahamu hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi ya Shirika.
 Meneja Msaidizi wa Miradi wa NHC, Etheldreder Koppa anayesimamia Mradi wa Victoria akitoa maelezo kwa wajumbe wa Menejimenti ya Shirika la Nyumba la Taifa waliofika katika mradi huo kufahamu hatua ya maendeleo ya mradi leo.
Violet Mafuwe ambaye ni mSanifu Majengo wa Kampuni ya CPI International ambaye pia ni Meneja wa Mradi wa Eco Residence akitoa maelezo kwa wajumbe wa Menejimenti ya Shirika la Nyumba la Taifa (hawapo Pichani) waliofika katika mradi huo kufahamu hatua ya maendeleo ya mradi leo.
 Meneja wa NHC Mkoa wa Dodoma, Itandula Gambalagi na Meneja wa Manunuzi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nyelu Mwamwaja wakiwa katika ziara hiyo kwenye mradi wa Victoria.
Jengo la Eco Residence katika picha
 Violet Mafuwe ambaye ni mSanifu Majengo wa Kampuni ya CPI International ambaye pia ni Meneja wa Mradi wa Eco Residence akitoa maelezo kwa wajumbe wa Menejimenti ya Shirika la Nyumba la Taifa (hawapo Pichani) waliofika katika mradi huo kufahamu hatua ya maendeleo ya mradi leo.

Afisa Mauzo wa Shirika la Nyumba la Taifa, Joseph Haule akitoa mwelekeo wa mauzo wa nyumba hizo za Shirika la Nyumba la Taifa.

No comments: