Friday, May 27, 2016

SHEREHE ZA KUAPISHWA KWA RAIS MPYA WA COMORO

Rais Mpya wa Muungano wa Comoro Mhe, Kanali Azali Assoumani Boinakheri akisalimiana na Viongozi wa Vikosi vya Ulinzi Comoro mara baada ya kuapishwa leo kwa kushinda uchaguzi mkuu wa April 10 na uchaguzi wa Marudio wa Mei 11 mwaka huu hafla ilifanyika leo uwanja wa Mpira Mjini Ngazija nchini Comoro
Vikosi vya majeshi ya Ulinzi vya Comoro vikitoa heshama kwa Rais Mpya wa Muungano wa Comoro Mhe, Kanali Azali Assoumani Boinakheri aliyeapishwa leo na jaji Mkuu wa Mahakama ya Katiba Mhe,Loutfi Soulaimane katika sherehe zilizofanyila uwanja wa mpira Mjini Ngazija nchini Comoro,
Makamo wa Rais wa Muungano wa Comoro Mhe,Jafar Ahmada Sais wa kisiwa cha Ngazija akiapishwa leo na Jaji wa mahakama ya katiba ya Nchi hiyo Mhe,Loutfi Soulaimane (hayupo pichani ) wakati wa sherehe za kuapishwa Rais kanali Azali na makamo wake 3 iliyofanyika leo baada ya ushindi wa uchaguzi Mkuu uliofanyika Aprili 10 na marudio ya uchaguzi huo uliofanyika mwezi mei 11 mwaka huu,hafla ilifanyika uwanja wa mpira mjini Ngazija leo,Mei 26 2016.[Picha na Ikulu.]
Rais Mpya wa Muungano wa Comoro Mhe, Kanali Azali Assoumani Boinakheri akitoa hutuba yake katika sherehe za kuapishwa zilizofanyika leo kufuatia kushinda Uchaguzi Mkuu uliofanyika April Kumi (10) na uchaguzi wa marudio uliofanyika mey 11 mwaka huu,hafla ya sherehe ilifanyika uwanja wa mpira Mjini Ngazija nchini Comoro,
Rais Mstaafu wa Muungano wa Comoro Mhe,Dkt.Ikililou Dhoinine (kulia) akiwa na Rais Mpya wa Muungano wa Comoro Mhe, Kanali Azali Assoumani Boinakheri (wa pili kulia) mara baada ya kuapishwa akiwa na Makamo wake wawili Mhe,Abdullah Said Sharman (kushoto) wa Kisiwa cha Mwali na Mhe,Mustarigan Aboud wa Kisiwa cha Anjouan (wa pili kushoto) katika uwanja wa mpira mjini Ngazija nchini Comoro leo,
Rais Mstaafu wa Muungano wa Comoro Mhe,Dkt.Ikililou Dhoinine (kulia) akiwa katikapicha na Rais Mpya wa Muungano wa Comoro Mhe, Kanali Azali Assoumani Boinakheri mara baada ya kuapishwa leo baada ya kushinda uchaguzi Mkuu wa April kumi(10) na uchaguzi wa marudio wa mei kumi na moja mwaka huu hafla ilifanyika leo uwanja wa Mpira Mjini Ngazija nchini Comoro,
Rais Mpya wa Muungano wa Comoro Mhe, Kanali Azali Assoumani Boinakheri akitoa salamu kwa kikosi cha Bendera mara baada ya kuapishwa leo akiwa mshindi katika kushinda uchaguzi Mkuu wa April kumi(10) na uchaguzi wa marudio wa mei kumi na moja mwaka huu hafla ilifanyika leo uwanja wa Mpira Mjini Ngazija nchini Comoro

[Picha na Ikulu.]

No comments: