Saturday, May 28, 2016

WASHIND KUMI WA KWANZA WA PROMOSHENI YA MILLIONI 100 NA TUSKER FANYA KWELI UWINI WATANGAZWA

 Meneja Masoko wa bia ya Tusker Nandi Mwiyombela (kushoto) akitoa maelezo ya promosheni ya Milioni 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini wakati wa droo ya kwanza ya promosheni hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, pembeni yake ni afisa kutoka Bodi ya kusimamia Michezo ya kubahatisha nchini Humud Semvua.
 Meneja Masoko wa bia ya Tusker Nandi Mwiyombela (kushoto) akiongea kwa njia ya simu na mmoja wa washindi kumi wa kwanza wa promosheni ya Milioni 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini katika droo ya kwanza ya promosheni hiyo, akishuhudiwa na afisa kutoka Bodi ya kusimamia Michezo ya kubahatisha nchini Humud Semvua (katikati), pamoja na muongozaji wa shoo hiyo Abdallah Mwaipaya ambaye pia ni mtangazaji wa ITV wakati wa droo ya kwanza inarushwa moja kwa moja kupitia ITV.
 Meneja Masoko wa bia ya Tusker Nandi Mwiyombela akiokota kuponi ili kujua mmoja wa washindi kumi wa kwanza.
 Afisa kutoka Bodi ya kusimamia Michezo ya kubahatisha nchini Humud Semvua (katikati) akihakiki namba ya simu ya mmoja wa washindi kumi wa kwanza wakati wa shoo ya sroo ya kwanza ya promosheni ya Milioni 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini jijini Dar es Salaam.
Muendeshaji wa shoo ya Milioni 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini na Mtangazaji wa ITV Abdallah Mwaipaya akitoa maelekezo wakati wa shoo hiyo ambapo washindi kumi wa kwanza walitangazwa.


 Ni wiki mbili tangu promosheni ya TUSKER FANYA KWELI UWINI ilipozinduliwa kiaina yake mikoa miwili tofauti kwa wakati mmoja, Dar es Salaam na Moshi. Leo washindi kumi wamepatikana katika droo ya kwanza na ya kusisimua. Milionea hawa walitangazwa leo katika droo iliyorushwa moja kwa moja na kushuhudiwa na waangalizi kutoka Bodi inayosimamia michezo ya kuigiza Tanzania, wana habari nan a wahusika wakuu wa promosheni hii ambao ni timu nzima ya Tusker lager. 

Washindi kupitia maongezi ya simu walionesha mshangao na furaha kubwa kushinda kitita cha Tsh. 1,000,000 ambapo wamekiri hawakutegemea kupata kiasi hicho cha pesa kwa hivi karibuni. Ukiachilia mbali washindi wa kila wiki wanaopatikana kupitia droo pia wapo watumiaji wa bia ya Tusker wanaojipatia bia kibao za bure kila siku. Promosheni bado ina wiki tisa mbele.

Washindi kumi wa kwanza ni Rehema Matemba, Elias Poto, Deogratius Shayo kutoka Kilimanjaro, Vestina Mainde, Doru B. kutoka Morogoro,  Sebastian Joseph, Michael Mwinuka,  Albert Tarimo na Festo Silvester ambaye ameshinda Millioni 2 wote kutoka Dar es Salaam.

Akiongea kwa njia ya simu mshindi wa kwanza Rehema Matemba ambaye ni mfanyabiashara katika manispaa ya Moshi alishikwa na mshangao kwani hakutegemea na anaona kama ndoto kuwa mshindi wa Milioni 1 kutoka Tusker kwani alishiriki promosheni hii wiki moja iliyopita na kuwa kati ya wale waliobahatika.

Naye mshindi wa pili Albert Tarimo alielezea furaha yake na kuishukuru Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kuwajali wateja wake kwa kugusa maisha yao ambapo kila mara huja na promosheni za kuvutia kwa wateja wake. “Nilishiriki kujaza vocha ya promosheni hii nilipokua bar nakunywa bia yangu ya Tusker sikutegemea kushinda kwani siku zote huwa sina mazoea ya kushiriki mashindano yeyote yale, nafuraha sana ni mara yangu ya kwanza kushiriki na kuwa moja ya washindi. Milioni 1 niliyoipata itanisaidia kuwalipia wanangu ada za shule kwangu ni faraja sana imekuja kipindi ambacho nauhitaji mkubwa wa pesa.” Alisema Tarimo.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa Bia ya Tusker Nandi Mwiyombela alieleza kuwa promosheni hiyo iliypo maalum kwa watumiaji wote ina faida kubwa kwa watumiaji wa bia zao za Tusker kama ilivyoanza kwa wateja kumi wa kwanza leo ambao wameguswa kwa namna tofauti nay a kipekee. “Ikiwa tu hapa ni hatua za mwanzo za promosheni hii kumekuwa na zaidi ya washindi 1000 wa bia za bure na maelfu wameshashiriki. 

Tangu tuzindue Tusker Fanya Kweli Uwini wiki mbili zilizopita tumepata muamko mkubwa kutoka kwa wateja wetu. Leo tumepata washindi wetu kumi wa kwanza ambao watakabidhiwa million 1 kila mmoja na kufanya jumla ya Million 10 kutolewa wiki ya kwanza. “Alisema Nandi.

Aliongeza kuwa “promosheni ya Tusker Fanya Kweli Uwini inaendelea na tumebakiwa na wiki tisa, tunapenda kuwakumbusha wateja wetu kuwa bado tuna Million 90 na bia kibao za kushinadaniwa! Kutakua na shughuli mbalimbali za burudani kila wikend yaani Ijumaa na Jumamosi kipindi chote cha kampeni yetu katika bar mbalimbali nchi nzima, hivyo mjitokeze kwa wingi muweze kufanya kweli. 

Katika huu mwanzo mzuri wa promosheni yetu napenda kuwashukuru sana wateja wetukwa kutuunga mkono na walivyoipokea kwa mikono miwili promosheni hii ya Millioni 100 na Tusker Fanya Kweli na Uwini.” Aliongeza Nandi

Droo za promosheni hii zitaendeshwa kila wiki na hiyo italeta msukumo kwa wateja na watumiaji wa bia ya Tusker kushiriki zaidi. Kwa utofauti kabisa hii ni promosheni ya kwanza iliyoangalia na wahudumu wa bar pia ambapo wahudumu watapata Tsh 100,000 endapo aliyemuhudumia akishinda. Hivyo leo washindi kumi wamepata Million 1 kila mmoja na wahudumu kumi pia wamepata 100,000 kila mmoja. 

No comments: