Sunday, May 29, 2016

NAPE AENDELEA KUKUTANA NA WANANCHI WA VIJIJI VILIVYOPO NDANI YA JIMBO LAKE AAHIDI KUMALIZA AHADI ZAKE MAPEMA


Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kijiji cha Kilimanjaro kilichopo kata ya Mtumbya ikiwa muendelezo wa mikutano yake ya kila kijiji katika jimbo lake ambapo alizungumzia utekelezaji wa ahadi alizoahidi na kuwahakikishia wananchi hao kuwa ahadi zake zitakamilika mapema mno.
Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiongozana na wakazi wa kijiji cha Kilimanjaro kilichopo kata ya Mtumbya kwenda kujionea maendeleo ya ujenzi wa zahanati.
  Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiangalia maendeleo ya ujenzi wa zahanati ya wanakijiji cha Kilimanjaro kilichopo jimbo la Mtama , wilaya ya Lindi Vijijini.
  Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiwasomea wakazi wa kijiji cha Mtumbya vijiji vitakavyopata umeme wa mradi wa umeme vijijini ( REA) awamu ya tatu katika jimbo la Mtama.
Mkazi wa kijiji cha Mtumbya Bw. Subiri Hashimu Saidia akiuliza swali wakati wa mkutano wa  Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye na wananchi hao.
Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akisalimiana na wakazi wakijiji cha Mpenda, Mtama
Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kijiji cha Mpenda ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa barabara ya kutoka Mtama, kupitia Mpenda , Mtumbya kwenda Kilimanjaro mkandarasi ameshapatikana na ataanza kazi hiyo mara moja na kuwahakikishia kuwa pamoja na kuwepo miradi mikubwa ya maji lakini Mpenda na Kilimanjaro watapata visima mapema.

No comments: