Wednesday, May 11, 2016

MAMA YAKE TEDDY MAPUNDA MAREHEMU BENADETTE IZENGO AZIKWA MAKABURI YA KINONDONI DSM

Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanania Dk. Gharib Bilal wa tatu kutoka kushoto na Mama Salma Kikwete wa kwanza kushoto wakishiriki mazishi ya Merehemu Benadette Izengo mama wa Mkurugenzi wa kampuni ya Montage Limited Teddy Mapunda aliyekaa katikati yao pamoja na wanafamilia wengine wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam baada ya ibada ya mazishi iliyofanyika kwenye kanis kuu la Mtakatifu Joseph. 
Mke wa Rais Mstaafu Dk Jakaya Kikwete Mama Salma Kikwete akiweka mchanga kaburini wakati aliposhiriki mazishi ya Marehemu Mama Benadette Izengo yaliyofanyika jana kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
Balozi Asha Rose Migiro akiweka mchanga kaburini wakati wa maishi ya marehemu mama Benadette Izengo.
Fathre Matumaini akiongoza ibada ya mazishi ya Marehemu Mama Benadette Izengo iliyofanyika kwenye kanisa la Mtakatifu Josepha jana.
Wanafamilia wakiwa katika ibada ya mazishi iliyofanyika kwenye kanisa la Mtakatifu Joseph jana jijini Dar es salaam na kufuatiwa na mazishi yaliyofanyika kwenye makaburi ya Kinondoni.
Teddy Mapunda na Ndugu yake wakiwa pembeni mwa jeneza la mama yao mpendwa marehemu Benadette Izengo.
Mkwe wa Marehemu mama Benadette Izengo akishiriki ibada ya mazishi pamoja na ndugu na jamaa wa familia kwenye kanisa la Mtakatifu Joseph jana.
Wajukuu wa marehemu wakishiriki ibada hiyo jana.
Wana familia wakiwa na majonzi kwa kuondokewa na mpendwa mama yao Marehemu Mama Benadette Izengo.
Mwenyekiti wa Chama cha UDP Mzee Jon Momose Cheyi akishiriki sakramenti ya bwana kutoka kwa Father Kaombwe wakati wa ibada hiyo ya mazishi
Teddy Mapunda na Mumewe Nestor Mapunda wakiwa na majozni huku wakiangalia jeneza la mama yao mpendwa marehemu mama Benadette Izengo.
Baadhi ya waombolezaji wakishiriki mazishi kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
Kutoka kushoto ni Jeseph Kusaga Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Enertainment, Nandi Mwiyombela, Justin Pamba, Godfrey Kusaga na John Mbele nao walishiriki katika mazishi hayo ya mama Bebadette Izengo.

No comments: