Thursday, May 05, 2016

NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI DK. MHANDISI JU.LIANA PALLANGYO AKUTANA NA WATENDAJI KUTOKA TPDC

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Dk. James Mataragio (mbele) akielezea mikakati ya shirika hilo katika matumizi ya  gesi asilia inayozalishwa kwa ajili ya matumizi ya majumbani na nyingine kuuzwa katika soko  la nje katika kikao kilichokutanisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati,  Dk. Mhandisi  Juliana Pallangyo  kilichofanyika  jijini Dar es Salaam. Lengo la kikao  hicho lilikuwa ni kujadili matumizi ya gesi iliyogunduliwa nchini katika matumizi  ya ndani na  nyingine kuuzwa nje ya nchi.
pal2Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati, Dk. Mhandisi Juliana Pallangyo (pichani) akisisitiza jambo  katika kikao hicho.
pal3Wataalam kutoka Idara ya Nishati kutoka kushoto, Mussa Abbas na  Athur Lyatuu wakinukuu  hoja mbalimbali zilizokuwa zinajadiliwa katika kikao hicho.
pal4Wataalam kutoka Idara ya Nishati iliyopo chini ya Wizara ya Nishati na Madini wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika kikao hicho

No comments: