Tuesday, February 02, 2016

FASTJET YAONGEZA NDEGE YA TANO

 
Dar es Salaam, Januari
28, 2016
-Fastjet
Tanzania imeongeza ndege nyingine aina ya Airbus A319 kwenye  idadi ya ndege zake nne  na hivyo kuliweka shirika hilo la ndege la
gharama nafuu kuendelea na mipango yake ya kupanuka.
“Ndege
za fastjet kwa hivi sasa ni nne na zote zinatumika  na ongezeko la ndege ya tano  ni jibu kwenye mikakati yetu ya  kupanuka pamoja na hitaji la kuongeza uwezo
wa kubeba kwenye safari zetu za ndani na za kimataifa”, alisema  Meneja Mkuu wa fastjet Tanzania, John Corse.
Ndege hiyo ya nyongeza  inafanya jumla ya
nafasi inayokuwepo kwa siku kwenye safari kwa ajili ya wateja kufikia 1,000.
Fastjet ilianza safari zake nchini mwaka 2012na hivi sasa inajiendesha kwa kutumia
ndege tano  aina ya A319 kwenye mtandao
wake wa safari ambao unahusisha Dar es Salaam, Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro na
Zanzibar na kuifanya ijikite kuufanya usafiri wa anga ndani ya Tanzania watu
wote waumudu.
Hali kadhalika ilianzisha safari za kimataifa
kwenda Entebbe nchini Uganda, Nairobi Kenya,  Harare Zimbabwe, Johannesburg Afrika Kusini
na Lusaka nchini Zambia katika kipindi cha miaka mitatu ya kuendesha shughuli
zake.
“Tangu tuanze safari zetu  tumeshabeba abiria
zaidi ya 1,800,000 ambapo utafiti wetu unaonesha kuwa  zaidi ya theluthi moja  ya abiria wetu walikuwa ndio mara yao ya kwanza
kumudu  kusafiri kwa ndege”, anasema
Corse.
Aliendelea kusema, “kuongeza ndege  nyingine  kwenye safari zetu  kunatupa fursa muhimu ya kuongeza masafa kwa  njia zetu zilizopo  ili kukidhi
mahitaji ya wateja, na na inasaidia kwenye lengo letu la kuongeza njia
moja ya kimataifa kwenye mtandao wetu kwa mwaka huu 2016”.
Hali kadhalika, Corse anabainisha kuwa  ndege
hiyo mpya  inamanisha kuwa fastjet ni sawia
na ni kubwa katika kutosheleza kupanuka kwa shughuli za fastjet.
Ndege hiyo A319  ambayo ni Airbus  ni ya injini mbili  ambazo zinatoa kiwango cha juu cha ufanisi
pamoja na kiwango cha chini kabisa cha madhara kwenye mazingira, ikiwa ni
nyongeza kwenye  viwango vya juu vya hali
ya kuliwaza ndani ya ndege hiyo ya kisiasa.
Ndege hiyo ina uwezo wa kubeba  abiria  156 ambaop wanamudu viwango vya chini vya
kuendesha mtindo wa maisha wa gharama nafuu ambao unaendeshwa na Fastjet
Tanzania.
Baadhi ya  njia muhimu ambazo ndege hiyo mpya
itakuwa inahudumia  ni njia mpya iliyoanzisjhwa hivi karibuni kati ya Dar es Salaam na Nairobi, Kilimanjaro na Nairobi  na Dar es Salaam kwenda Zanzibar ambazo zote zilianza kwa mara ya kwanza Januari 11, 2016. njia hizi mpya  zote ni kielelezo muhimu muda mrefu kwenye
upanuzi wa  njia za fastjet kitaifa na
kimataifa.
Fastjet inatarajia kuongeza ndege zaidi kwenye njia yake ya Kenya  kutokana na mahitaji ya wateja kuongezeka kunakosababisha na kumudu, usalama, kasi na huduma kwa wakati, na hali
kadhalika  imeshajionesha kuwa  kuna matarajio ya  kuzindua
safari kati ya Zanzibar na Nairobi
na hali kadhalika kati ya Dar es Salaam na Mombasa baadaye mwaka 2016.
“Usafiri wa anga unaoumudu ni muhimu kwenye  kukuza uchumi wa Tanzanoa, hususani kwenye   kukuza sekta za biashara na utalii”, alisema
Corse.
Hali  kadhalika Corse alibainisha  kuwa ndege hiyo mpya inamaanisha kwamba ndege za
Fastjet zitatosheleza kiasi cha kutosha  kusaidia kwenye changamoto za usimamizi na uendeshaji  iwapo
ndege moja miongoni mwake  itakuwa haifanyi kazi au kama ipo kwenye matengenezo au ukarabati wa lazima.

No comments: